• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Ripoti zasema Yevgeny Prigozhin wa Wagner ameangamia

Ripoti zasema Yevgeny Prigozhin wa Wagner ameangamia

NA MASHIRIKA

MOSCOW, Urusi

KIONGOZI wa Mamluki wa Wagner Yevgeny Prigozhin ni miongoni mwa watu 10, ambao inahofiwa wameangamia baada ya ndege ya kibinafsi waliokuwa wakisafiria kudaiwa kuangushwa katika eneo la Tver nchini Urusi.

“Ndege ya kibinafsi aina ya Embraer Legacy iliyokuwa ikisafiri kutoka Moscow kyenda Petersburg ilianguka karibu na kijiji cha Kuzhenkino katika eneo la Tver. Kulikuwa na abiria 10 humo wakiwemo wahudumu watatu,” Wizara ya Majanga ikasema kwenye taarifa fupi kupitia mtandao wa Telegram.

“Uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa abiria wote waliokuwa humo walikufa,” taarifa hiyo ikaongeza.

Lakini shirika la habari la Urusi TASS ndilo liliripoti kuwa Prigozhin, ambaye ni kiongozi wa kundi la wapiganaji wa kukodishwa la Wagner, alikuwa miongoni mwa waliokuwa kwenye ndege hiyo.

Baadaye duru zilisema kuwa huenda ndege hiyo ilidunguliwa.

Mnamo Juni 2023, kundi la Wagner lilitishia utawala wa Rais wa Urusi Vladimir Putin lilipofululiza ndani ya kambi ya kijeshi likilenga kufanya mapinduzi ya wakuu wa jeshi.

TAFSIRI: CHARLES WASONGA

  • Tags

You can share this post!

Njeri Maina aambiwa angetafuta matibabu hospitali ya...

Ruto: Tutajenga studio za kisasa katika kila kaunti

T L