• Nairobi
  • Last Updated April 27th, 2024 6:00 PM
Balozi wa Uganda nchini Kenya afariki jijini Nairobi

Balozi wa Uganda nchini Kenya afariki jijini Nairobi

NA DAILY MONITOR

BALOZI wa Uganda nchini Kenya na Ushelisheli, Dkt Hassan Wasswa Galiwango, amefariki akiwa jijini Nairobi, serikali ya taifa lake imethibitisha.

Amefariki akiwa katika hospitali moja jijini Nairobi.

Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza Rebecca Kadaga amethibitisha hayo leo Jumatatu.

Dkt Galiwango aliteuliwa kuwa balozi mnamo Oktoba 2020 kuchukua nafasi ya Phibby Otaala aliyekuwa na azma ya kuwania kiti cha kisiasa nchini mwao.

Aliwasilisha karatasi zake za uteuzi kwa aliyekuwa Rais wa Nne wa Kenya Uhuru Kenyatta mnamo Machi 3, 2021.

Aidha Galiwango aliwahi kuwa mkurugenzi wa masuala ya fedha na usimamizi katika sekretarati ya chama tawala nchini Uganda, National Resistance Movement (NRM).

Marehemu alikuwa mume wa Mbunge wa Kike wa Mbale City, Connie Nakayeze Galiwango.

  • Tags

You can share this post!

Nafasi za Kidato cha Kwanza kujulikana leo Jumatatu

Pesa za wazee sasa ni mtego wa mauti

T L