• Nairobi
  • Last Updated May 13th, 2024 3:09 PM
Dalai akemewa kwa kutaka mtoto amnyonye ulimi

Dalai akemewa kwa kutaka mtoto amnyonye ulimi

NA MWANDISHI WETU

CARDI B, mwimbaji wa nyimbo za rapu nchini Marekani amemkashifu vikali Dalai Lama, kiongozi wa kidini wa Watibet kwa kumtaka mtoto kumnyonya ulimi.

Kwenye ujumbe wake kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter, Cardi B alimfokea Lama akisema kuwa dunia imejaa wanyanyasaji wanaowaendea hata watoto.

Aliongezea kuwa wanyanyasaji hawa wa kimapenzi huwa majirani, walimu shuleni, watu wenye pesa zao au mamlaka hata kanisani.

“Kuwa ukimzungumzia mwanao kila wakati kuhusu mipaka ambayo wanapaswa kuwawekea watu ili wasije wakaumizwa,” akasema.

Dalai Lama, kiongozi wa kidini wa Watibet afokewa kwa kumtaka mtoto kumnyonya ulimi. PICHA / HISANI

Video ya Lama, 87, ilienea mitandaoni wikendi hii iliyopita huku watu wakikashifu kitendo chake cha kumtaka mtoto wa kiume kumnyonya ulimi.

Video hiyo ilionyesha Lama akimbusu kijana huyo kisha akatoa ulimi wake na kumweleza aunyonye.

Tabia ya kiongozi huyo wa kidini, imezua mdahalo mkali mitandaoni wanamitandao wakishangaa ni kwa namna gani kiongozi wa hadhi yake anaweza kufanya kitendo cha aina hiyo kwa mtoto.

Huku watu wakimkashifu, Lama aliomba msamaha na kuchapisha ombi hilo kupitia ukurasa wake wa Twitter.

“Lama anamuomba msamaha kijana huyo, wanafamilia wake pamoja na marafiki duniani kote kwa matamshi aliyotoa.”

Tukio hilo lilirekodiwa mwishoni mwa mwezi wa Februari katika sherehe mji wa Dharamshala, India Kasakazini.

  • Tags

You can share this post!

Kocha Mulee asema Gaspo Women wameweka macho kwa Kombe la...

Kaunti yatoa tahadhari watoto wengi wakiugua Rotavirus

T L