NA MASHIRIKA
KINSHASA, DRC
JAMHURI ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) inaendeleza hatua za mwisho mwisho kukamilisha ujenzi wa mnara wa kumkumbuka waziri mkuu wa kwanza wa taifa hilo, Patrice Lumumba.
Mnara huo ni wa kipekee, kwani utakuwa na jino la dhahabu la kiongozi huyo.
Jino hilo ndilo sehemu ya pekee ya mwili wa kiongozi huyo ambayo iliyopatikana baada ya mauaji yake mnamo 1961.
Jino hilo limepangiwa kurudishwa kwa familia yake kwenye hafla maalum itakayofanyika jijini Brussels, Ubelgiji.