• Nairobi
  • Last Updated April 30th, 2024 1:01 PM
Kongamano kuhusu ajenda ya afya kuandaliwa jijini Kigali mnamo Machi 5-8

Kongamano kuhusu ajenda ya afya kuandaliwa jijini Kigali mnamo Machi 5-8

Na PAULINE ONGAJI

KONGAMANO la Kimataifa kuhusu ajenda ya afya barani Afrika (AHAIC 2023) litaandaliwa kati ya Machi 5 na Machi 8, 2023 mjini Kigali, Rwanda.  

Kongamano hili limeandaliwa kwa ushirikiano wa shirika la Amref Health Africa, Wizara ya Afya nchini Rwanda, Muungano wa Afrika na Africa CDC.

Haya yakiwa Makala ya tano, kongamano hili litaleta pamoa baadhi ya viongozi wakuu barani, wanasiasa, wavumbuzi, watafiti, wahudumu wa kiafya, miongoni mwa washikadau wengine katika sekta ya afya, ili kujadili jinsi ya kujadili mwelekeo wa kuunganisha masuala ya tabianchi na sera za kiafya.

Kulingana na Desta Lakew, mkurugenzi wa masuala ya nje katika shirika la AMREF, kwa mara ya kwanza kongamano hili litatoa fursa ya kuchambua athari za tabianchi katika afya.

“Azimio kuu litakuwa usalama wa masuala ya kiafya. Tunatambua kwamba mabadiliko ulimwenguni katika kipindi cha mwongo mmoja ujao yatazungukia masuala ya tabianchi na afya,” aliongeza.

Kama mojawapo ya mikutano mikuu ya kiafya mwaka huu, kongamano hili aidha litatoa jukwaa la kujadili masuala ambayo yameratibiwa kuzungumziwa katika bunge la Afya ulimwenguni, Bunge kuu la Unoja wa Mataifa (UNGA) na kongamano la 2023 la Umoja wa Mataifa kuhusiana na mabadiliko ya tabianchi, al-maarufu COP28 mwaka huu.

Tangu mwaka wa 2014, kongamano hilo ambalo huandaliwa kila baada ya miaka miwili limekuwa likihusisha washikadau katika masuala ya kiafya kutoka barani Afrika, ili kuzungumzia masuala ya afya, kuunda msingi wa ushirikiano wa mataifa yenye mapato ya chini, na kumarisha mifumo thabiti ya afya.

Kongamano la mwisho la AHAIC lilifanyika 2021 kwa njia ya mtandaoni kutokana na marufuku ya usafiri yaliyotokana na maradhi ya COVID 19 ambapo zaidi ya washiriki 3,000 walihusika.

Katika hafla hiyo, shirika la Amref Health Africa lilizindua tume huru ya kukagua hatua ambazo mataifa ya Afrika zimepiga katika kutimiza ndoto ya Afya kwa wote (UHC) kufikia mwaka wa 2030.

Hii ilifuatiwa na uchapishaji wa ripoti ya The State of UHC in Africa, iliyotoa kwa kina hatua ambazo serikali za Afrika zimechukua katika kutimiza UHC.

  • Tags

You can share this post!

UJASIRIAMALI: DJ anayekupa burudani aali akijihakikishia...

Mung’aro apumua kesi dhidi yake ikitupiliwa mbali

T L