• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Muuzaji mitishamba akamatwa kwa kuuza dawa zilizopigwa marufuku

Muuzaji mitishamba akamatwa kwa kuuza dawa zilizopigwa marufuku

NA DAILY MONITOR

KAMPALA, UGANDA

MUUZAJI mmoja wa mitishamba nchini Uganda amekamatwa kwa kupatikana akiwa na dawa zilizopigwa marufuku na ambazo inadaiwa ni za kuongeza hamu ya kufanya mapenzi.

Kulingana na polisi, dawa hizo zilipigwa marufuku na Mamlaka ya Kitaifa ya Dawa (NDA) kutokana na athari zake kwa watumizi.

Mbali na dawa hizo za kusisimua hamu na nguvu za kushiriki mapenzi, alipatikana na dawa zinazodhibitiwa za upangaji uzazi.

Pia inadaiwa amekuwa akipeana habari na maelezo ya kupotosha kuhusu matumizi ya dawa hizo.

“Rashid Ashiraf Lukwago alikamatwa kwa kuwahadaa watu kununua dawa alizodai zinaongeza nguvu za kiume. Dawa hizo zilipigwa marufuku ila akaendelea kuziuza,” ikasema NDA.

  • Tags

You can share this post!

Tamaa ya visketi ilivyomponza Greenwood hadi akachujwa Man...

Nitakupa kiti cha Kiongozi wa Upinzani ndio uache...

T L