Na AFP
WATU waliojihami vikali Jumapili walimuua afisa wa polisi na kuwateka nyara raia watano wa China, waliokuwa wakifanya kazi katika mgodi mmoja wa dhahabu katika Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo.
Jeshi lilisema kisa hicho kilifanyika katika eneo la mashariki, linalokumbwa na mapigano.Msemaji wa Jeshi katika eneo hilo, Meja Dieudonne Kasereka, alisema kisa hicho kilifanyika mwendo wa saa nane usiku.