• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 6:55 PM
Ajabu mwanamke mgonjwa akitapika panya eneo la Nakuru

Ajabu mwanamke mgonjwa akitapika panya eneo la Nakuru

SAMMY WAWERU na MASHIRIKA  

MWANAMKE anayeugua Kaunti ya Nakuru amegeuka kuwa gumzo la mtaa baada ya kutapika panya.

Duru zinaarifu mama huyo alitapika panya aliyefariki, kufuatia tukio hilo la Jumatano, Juni 28, 2023.

Kisa hicho kilifanyika katika Kijiji cha Ndaragu, Njoro, Kaunti ya Nakuru.

Inasemekana mwanamke huyo ambaye ni mama wa watoto wanne amekuwa mgonjwa kwa muda wa wiki moja.

Alisema alianza kuhisi vibaya usiku kabla ya tukio, kisha akaanza kutapika.

“Mwendo wa saa tisa hivi za asubuhi, nilihisi kitu kama kifaa kwenye koo na baada ya kukilazimisha kitoke (kwa njia ya kutapika) nilishangaa kuona ni panya aliyefariki,” alisimulia wanahabari.

Babake na mzee wa kijiji walisema kabla ya kisa, mwanamke huyo alikuwa ametofautiana na jamaa fulani.

Walishuku huenda akawa ndiye chanzo cha mama huyo kutapika panya aliyekufa.

Hata baada ya tukio, mwanamke huyo alirejea kulala wanakijiji asubuhi ya siku iliyofuata wakifurika katika boma lao baada ya babake kupasua mbarika ya yaliyojiri.

Kwa mujibu wa mila, itikadi na tamaduni za jamii ya mama huyo, wazee wanatarajiwa kufanya matambiko.

Matambiko hayo yanatarajiwa kusafisha yaliyofanyika, na hata kuondoa laana.

Kwa baadhi ya jamii, tukio la aina hiyo linafasiriwa kama laana.

  • Tags

You can share this post!

Mary wa Maua asimulia ugumu kumpoteza mwandani spesheli kwa...

Mgomo: Shughuli za usambazaji maji zatatizika mjini Malindi

T L