• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Amina Khalef amlilia Ali Kiba kutia saini stakabadhi za talaka

Amina Khalef amlilia Ali Kiba kutia saini stakabadhi za talaka

NA MERCY KOSKEI

MKE wa staa wa Bongo, Ali Kiba kutoka nchini Kenya, Amina Khalef amevunja kimya chake kuhusu ndoa yake na mwimbaji huyo.

Wawili hao wamekuwa pamoja kwa miaka mingi baada ya kufanya harusi mbili za kifahari Mombasa na Dar es Salaam, ambazo ziliripotiwa kugharimu mamilioni ya pesa.

Kupitia kwa mtandao wake wa Instagram ,Bi Khalef alichapisha nakala juu ya hali yake ya talaka akibainisha kuwa alikuwa amechoshwa na ukosefu wa heshima uliotokana na kuishi kama mke wa Kiba.

Alitaja  kupuuzwa kuwa sababu ya kuwasilisha talaka yake.

“Nimeona haja ya kushughulikia hili suala kwa vile linakuwa  gumu na haliwezi kuvumilika. Nimechoka kudharauliwa hadharani kwa kuwa watu hawaelewi nini hutokea unapoishi kwenye kivuli cha mtu kama mke wake,” alisema

Amina alifichua kuwa alitoka katika maisha ya Ali Kiba ili kukwepa maumivu na unyanyasaji.

“Nilitoka maishani mwako ili kuepuka maumivu na unyanyasaji, lakini hadi leo, hutaki kunipa talaka, unaishi kama mtu huru na unafanya upendavyo, lakini bado umeniacha niishi kwenye kivuli chako kama mke wako ukisema kuwa unachunga brandi yako,” aliongeza

Alimsihi mwimbaji huyo kutia saini stakabadhi za talaka.

“Tafadhali saini hati za talaka ili nipate talaka yangu na kila mtu aweze kuishi uhuru.”

Mnamo 2022, mke wa Ali Kiba, Amina Khalef, aliwasilisha kesi ya talaka baada ya miaka mingi ya ndoa yao ya furaha, akitaja mafadhaiko na kutelekezwa.

Amina alikuwa amewasilisha talaka katika Mahakama ya Kadhi ya Mombasa na alikuwa akitaka Sh 200,000 kama malipo ya kila mwezi.

 

 

  • Tags

You can share this post!

Makahaba Thika wapandisha bei ya huduma, wakilalamikia...

Guardian Angel ajigamba kuishi Karen

T L