• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 6:09 PM
Andrew Kibe akaangwa na wafuasi wake mitandaoni

Andrew Kibe akaangwa na wafuasi wake mitandaoni

NA FRIDAH OKACHI

MTANGAZAJI wa zamani na mwanakotenti Andrew Kibe hatimaye ameweka paruwanja kuhusu familia yake, jambo ambalo limeonekana kuwa kinaya cha msimamo kuhusu ndoa ikizingatiwa kuwa amekuwa akihimiza vijana kutopata jiko.

Bw Kibe amekuwa mkosoaji mkuu wa wenye nia kuingia kwenye ndoa n ahata waliooleka.

Licha ya msimamo wake, mwanakontenti huyo ameweka wazi – kupitia picha aliyopakia kwenye akaunti yake ya X (awali Twitter), akiwa na wanawe wawili.

Mtangazaji huyo wa zamani wa redio alichapisha picha hiyo baada ya kurejea nchini, Kenya. Kibe, amekuwa akiishi Amerika.

“Na matunda ya mwili wangu,” Kibe aliandika, picha ikiashiria pamoja na wanawe walijawa furaha.

Aidha, picha hiyo imevutia hisia mseto miongoni mwa wafuasi wake wakifurika kwenye safu ya maoni.

“Kumbe gaidi inakuanga na watoi (watoto) na kazi ni kutuambia tuachane na wanawake,” alichangia Super Metro.

“Kwa hiyo una watoto na bado unakatiza tamaa za watu kuoa,” alishangaa Kijana Yaa.

Shabiki kwa jina Eye witness alichangia akisema kumbe nasaha ambazo amekuwa akitoa zilikuwa mchezo.

“Na vile wanaume wengi wamekuwa wakimsikiza, aa!!! Huu ulikuwa mzaha,” alisema Eye Witness.

Kibe amekuwa mshauri wa masuala ya ndoa, baadhi ya semi zake zikimweka kwenye kikaangio moto.

Msanii Esther Akoth maarufu kama Akothee alipofunga pingu za maisha na mchumba wake Dennis Schweizer (japo waliachana) Aprili 2023, Kibe alimkosoa jambo ambalo lilionekana kukera mwanamuziki.

Kibe amekuwa akionya vijana kuhusu ndoa, akihimiza waliooa na kujaaliwa kupata watoto kuhakikisha wanafanya vipimo vya msimbojeni (DNA) kubaini ikiwa ni wanao halali.

 

  • Tags

You can share this post!

Wahuni wa utekaji nyara Kiambu wanaswa   

DJ Saint Kevin: Karen Nyamu anaelewa kupenda  

T L