NA SAMMY WAWERU
IDARA ya Kitaifa ya Huduma za Polisi (NPS) imepata mgao wa Sh800 kusaidia kuboresha magari.
Waziri wa Fedha na Hazina ya Kitaifa, Prof Njuguna Ndung’u alisema Alhamisi, Juni 15, 2023 wakati akisoma Makadirio ya Bajeti 2023/24, mgao huo utasaidia idara ya polisi kuimarisha huduma za usalama kwa umma.
“Hali kadhalika, Idara ya Polisi itapata mgao wa Sh850 milioni kuboresha maabara ya uchunguzi na utafiti wa kiusalama,” Prof Ndung’u alielezea.
Rais mstaafu Uhuru Kenyatta, kabla kustaafu 2022 alizindua maabara ya kisasa katika makao makuu Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI).
Kwa muda mrefu, maafisa wa polisi wamekuwa wakilalamikia upungufu wa magari kuendeleza huduma za usalama kiasi cha kushinikiza umma kutoa pesa kugharamia mafuta.