• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Akothee aliyeoga na kurudi soko, ametwaliwa tena na ‘Ex’ Nelly Oaks?

Akothee aliyeoga na kurudi soko, ametwaliwa tena na ‘Ex’ Nelly Oaks?

Na MERCY KOSKEI

MWANAMUZIKI Akothee amewaacha wanamitandao na maswali mengi ikiwa wamerudiana na meneja wake wa zamani, Nelson Oyugi almaarufu Nelly Oaks baada ya kuposti video kadhaa wakiwa pamoja.

Wawili hao wameonekana wakiwa pamoja mara kadhaa hivi majuzi ikiwa ni Nairobi na Migori, wakistarehe na kuwacha wengi wakikisia walirudiana.

Mama huyo wa watoto watano amekuwa akiposti video kwa mitandao yake ya kijamii akiwa na Nelly akimtembeza katika kaunti hizo mbili.

Mnamo Novemba 15,2023 Akothee alishiriki video kwenye mtandao wake wa Instragram, akiendesha gari na Nelly jijini Nairobi huku wakirushiana mistari ya mapenzi.

Kwenye video hiyo, Akothee aliyejipa taji la Rais wa Wanawake ambao Hawajaolewa, alionekana akijipendekeza huku akijipaka vipodozi, na alipomuuliza Nelly ako vipi.

“Unaonekana kama almasi,” Nelly alimjibu.

Akothee alicheka na kumwambia Nelly:

“Ninakupenda ukiwa umevaa nguo nyeupe, unaonekana vizuri.”

Baadaye, Akothee aliposti video nyingine ya Nelly akimchukua katika Uwanja wa Ndege wa Wilson, Nairobi, na kuacha mashabiki wake wakiwa wamechanganyikiwa.

Katika video hiyo alinukuu: “Yeye hunichukua baada ya mikutano.”

 Wengi walifurika kwenye safu ya maoni huku wakisema kuwa Akothee na Nelly wanafaana huku wakimsifu kwa kuwa mwanaume kamili.

“Saa hii Nelly Oaks ndio mambo yote baada ya kuachwa na Omosh,” Jackycharles419 aliandika.

“Kwa hiyo nyie mmerudiana? Karibu tena Nelly,”  Princess Sunday alisema.

“Nampigia saluti Nelly bado alimchukua baada ya mabaya yote aliyoyasema juu yake baada ya kumpata Omosh,” Jeronogetrude alisema.

Akothee walitengana na mumewe mzungu Denis ‘Omosh’ Shweizer baada ya wawili hao kufunga ndoa Aprili.

  • Tags

You can share this post!

Mwanamke ashtakiwa kutwaa bidhaa baada ya mwanamume...

Raila afichua ‘bonge la skendo’ kuhusu kile...

T L