• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
Bila shamba la ekari 50 hutamuoa Awinja, waume wanaommezea mate waambiwa

Bila shamba la ekari 50 hutamuoa Awinja, waume wanaommezea mate waambiwa

NA FRIDAH OKACHI

MWIGIZAJI na mwanakotenti Jacky Vike almaarufu Awinja, ameweka wazi anahitaji mwanamume atakayemuoa ila atahitaji kuona ardhi yenye ekari 50 ili kutimiza ndoto yake ya kuishi mashambani.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mcheshi huyo alipakia video akiwa kijijini akiwachunga ng’ombe, mbuzi huku akitembea kwenye shamba lenye mahindi. Ndoto yake ikiwa ni kumiliki shamba kubwa.

Alidai iwapo kunaye mwanamume aliye na matamanio ya kumpenda lazima awe na ekari 50 za shamba.

Mwigizaji huyo alisema nia yake kuwa kwenye ndoa ni kufanya kilimo na kuishi mashambani.

“Niseme mapema yule atanioa, haya ndio maisha ninayotaka. Sitaki vitu vingi, ekari 50 za ardhi tu,” alichapisha Awinja.

Mcheshi huyo anajiunga katika orodha ya wanawake wanaotambulika nchini Kenya kutangaza bei ya mahari yao hadharani.

Mapema Novemba 2023, sosholaiti Mylee Stacy alitangaza thamani yake ifikiayo Sh800 bilioni.

Mwanakotenti Eve Mungai alianzisha suala hilo la kutolewa mahari ya kima cha Sh10 milioni.

Kwenye ukurasa huo, mashabiki wake walimkashifu kwa kutoa masharti hayo ya kuolewa.

“Aaii…Kenya ina shamba, inatoka wapi?…hiyo ni trilioni anataka…Je, wewe unatosha trilioni?” alisema Silvester K.

Wengine walitoa hoja zao wakitaka wanawake wajitume kufanya kazi kutokana na hali ya wanaumume dhaifu wanafanya maisha kuwa magumu na iwapo unataka kitu, itakuwa vyema kutafuta pesa.

Pia, mcheshi huyo alihusishwa na jamii yake wakitoa madai kuwa jamii ya Waluhya hawaitishi vitu vya maana.

  • Tags

You can share this post!

‘Nililazimika kuacha shule nikaolewa, nikazaa watoto...

Raila asuka mbinu mpya ya kupambana na serikali

T L