• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 9:55 AM
Maswali Seneta Karen Nyamu akisaidia Samidoh kutumbuiza majuu

Maswali Seneta Karen Nyamu akisaidia Samidoh kutumbuiza majuu

NA MERCY KOSKEI

MASHABIKI wa msanii wa Mugithi, Samuel Muchoki almaarufu Samidoh nchini Australia  walishangaa kumuona Seneta maalum Karen Nyamu akimsaidia kutumbuiza. 

Wawili hao walifanya shoo katika mojawapo ya maeneo ya burudani nchini Australia na kuwaacha wengi kwa mshangao kwa jinsi wanavyopendana.

Nyamu alijumuika na mpenziwe jukwaani akiwaacha mashabiki wa Samidoh kwa furaha huku wakishangilia walipokuwa wakirekodi matukio.

Wakati wa onyesho hilo, Samidoh aliimba mmojawapo wa nyimbo zake maarufu, huku Nyamu, ambaye ni Seneta maalum akionyesha jinsi anavyojua kusakata densi.

Katika video iliyosambazwa kwa mitandao ya kijamii, Seneta huyo mteule alikua amevalia vazi fupi jeusi amabayo ilikua imembana na viatu vyekundu akiwa jukwani na staa huyo wa Mugithi.

Umati ulilipuka kwa shangwe huku wapenzi hao wakionyesha jinsi mapenzi baina yao imenoga.

Wakati wa onyesho hilo lisilosahaulika, Samidoh aliburuza hadhira kwa mojawapo ya nyimbo zake maarufu, sauti yake ya kupendeza ikisikika ukumbini

  • Tags

You can share this post!

Kenya yakaribia kujipatia Mtakatifu wake wa kwanza katika...

Mwanamume asimulia jinsi ulevi ulivyofanya apoteze kazi...

T L