• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 5:50 AM
Mcheshi Mtumishi afanyiwa patanisho na mamake

Mcheshi Mtumishi afanyiwa patanisho na mamake

NA FRIDAH OKACHI

MCHEKESHAJI Gilbert Barasa almaarufu Mtumishi alipatanishwa na mamake mzazi kupitia njia ya simu na mtangazaji Massawe Japanni.

Mchekeshaji huyo alikuwa amemlaumu mamake kwa kufanya ‘uchawi’ jambo alilosema lilimfanya baba mzazi kuondoka nyumbani na kuanza familia nyingine.

Alhamisi Novemba 16, 2023, mchekeshaji huyo alifurahi baada ya mtangazaji Massawe Japanni kumpigia mamake simu akitaka kufahamu maelewano baina yao yalipungua lini.

Katika simu hiyo, mama Mtumishi alishangaa kusemwa vibaya na mwanawe na kutupilia mbali madai ya uchawi yaliyoibuliwa.

“Mbona aniweke na kunianika  kwa ulimwengu mzima? Sitaki kuongea na yeye saa hii. Kama anataka tuongee, aje nyumbani mbele ya watu wetu,” alisema mama huyo.

“Alisema mimi ni mchawi, basi aje atoe huo uchawi? Ikiwa mimi ni mchawi, hata yeye ni mchawi. Kama ni kuongea aje mbele ya wazazi wangu na ndugu zangu,” aliendelea.

Mtumishi alifurahia kuzungumza na mama mzazi baada ya kukosa kuongea naye kwa muda wa miaka miwili. Vilevile, alijitetea na kusema hakuwa na nia yeyote ya kumshambulia na kumtangaza, akitaja ni hisia alizopata akiwa kanisani.

“Nimefurahi mama amesema tuende tuongee. Hivyo ndo nilikuwa nataka. Simchukii, nampenda.”

“Mimi sikuenda hadharani. Hisia ilikuja nilipokuwa kanisani kwa madhabahu na nikasema. Sio kitu nilikuwa nimepanga kusema. Niliskia tu imenitoka. Nimeishi nayo tangu nikiwa mtoto,” aliweka wazi Mtumishi.

Katika jaribio la pili la kumtafuta mamake Mtumishi kwa njia ya simu, mchekeshaji huyo aliomba msamaha huku mamaye akiwa mzuri na kumwambia mchekeshaji huyo atasalia kuwa mtoto wake.

“Mama, naomba msamaha lakini ningependa kujua kama nimewahi kukosea ili niombe msamaha,” aliomba Mtumishi.

Mchekeshaji huyo alishtua mashabiki wake kwa kile alichosema mamake ni mchawi na kwamba alichangia babake kuondoka kwenye familia yao. Pia, alimlaumu mamake kutokana na ndoa yake kuvunjika.

  • Tags

You can share this post!

Madai ya Raila kuhusu skendo ya mafuta ni ‘hot...

Anapigwa mawe akiyageuza gorofa: Diana Marua aingia orodha...

T L