• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 6:55 PM
Mkesha: DJ Fatxo kutumbuiza mkahawani Aberdare

Mkesha: DJ Fatxo kutumbuiza mkahawani Aberdare

NA MWANGI MUIRURI

WAKAZI wa Kaunti ya Nyeri na majirani wao wamealikwa na DJ Fatxo katika hafla ya mkesha wa kupisha Mwaka Mpya wa 2024 akiwatumbuiza kwa ngoma.

Kwa mujibu wa DJ Fatxo ambaye jina lake kamili ni Lawrence Njuguna Wagura,26, atakuwa katika Mkahawa wa Aberdare ulioko mjini Karatina.

“Hapo ni uje nikutumbuize ukijipa raha na tupishe mwaka mpya ambao tuna matumaini utakuwa na mafanikio tele,” akasema DJ Fatxo.

Akifahamika kwa ubunifu wake katika utunzi wa nyimbo na pia sauti yake ya kuvutia huku akiwa na weledi wa juu wa kucheza ala tofauti za muziki, taaluma yake ilipata pigo Mei 2023 alipoanza kuchunguzwa kwa madai ya kuhusika katika mauti ya mwanamitindo Jeff Mwathi.

Hata hivyo, vitengo mbalimbali vya maafisa wa usalama na upelelezi hatimaye vilimwondolea lawama vikisema kwamba kijana huyo alijitoa uhai kwa kuruka kutoka kwa nyumba ya msanii huo iliyo eneobunge la Kasarani katika orofa ya tano.

Ni kashfa ambayo ilitishia nyota ya DJ Fatxo lakini sasa anasema kwamba “licha ya kupakwa tope, Mungu alisimama na haki yangu na pia ya mwendazake”.

DJ Fatxo amekuwa akirejea sokoni polepole kwa umakinifu mkuu na kwa sasa ameonekana kujipamba upya akisaka mashabiki wapya.

[email protected]

  • Tags

You can share this post!

Sniper: Ripoti ya uchunguzi wa awali yatoka

Kuzubaa kwa sababu ya mihadarati kunasababisha ajali

T L