• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 PM
Rayvanny amwaga sababu za kujitoa WCB

Rayvanny amwaga sababu za kujitoa WCB

NA RAJAB ZAWADI

WIKI jana Rayvanny, Vanny Boy, alisherehekea mwaka mmoja tangu alipojiondoa kwenye lebo ya WCB Wasafi yake Diamond Platnumz.

Akipiga stori na stesheni moja ya redio kule kwao, bosi huyo wa lebo ya Next Level alitema nyongo sababu zake za kujiondoa WCB.

Rayvanny alisema sababu kubwa ya kutaka kuondoka ni kwa sababu alitaka kujiongeza kwa maana ya kukua.

“Ni hatua tu za kukua kwa kusonga kutoka sehemu moja kuenda sehemu nyingine. Kwa hiyo nikasema hatua niliyofikia ninaweza nikasonga mwenyewe na mimi nikashika mkono watu wengine na wala si kubaki na kuendelea kushikwa mkono,” akasema Rayvanny.

Hata hivyo, mwanamuziki huyo anasema kulikuwa na mvutano mkubwa sana alipomwambia Diamond kuhusu uamuzi wake huo.

Mwanamuziki Rayvanny akiwa jijini Nairobi, Kenya. PICHA | MAKTABA

“Kwanza tulikuwa tu kwenye stori za kawaida tukiwa pale kwake halafu nikamgusia (kwamba nataka kuondoka) kwa sababu namjua. Najua anajivunia sana mimi lakini pia kuna namna ambavyo mtu huwa. Mwanzoni hakulichukulia suala hilo poa lakini baadaye alielewa na hakuweka vikwazo vingi. Hata kama kulikuwa na mivutano na nini na nini, lakini tuliweza kumaliza na tukawa na mahusiano mazuri bado,” akaeleza.

Rayvanny aling’oka baada ya kuilipa WCB Sh68 milioni (za Kenya) ili kuvunja mkataba wake uliokuwa umesalia na miaka minne.

IMEKUSANYWA NA SINDA MATIKO 

  • Tags

You can share this post!

Waathiriwa wa mafuriko Lamu wapokea msaada

Kuria apinga agizo la Papa kubariki wapenzi wa jinsia moja

T L