• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 6:55 PM
Tiktoker Nyako kwa mara ya kwanza azungumzia giza lililogubika familia yao

Tiktoker Nyako kwa mara ya kwanza azungumzia giza lililogubika familia yao

NA FRIDAH OKACHI

‘TIKTOKER’ Roseline Ngolo almaarufu Nyako Pilot, amezungumzia jinsi alivyowapoteza wazazi wake na dada wawili kutokana na ugonjwa.

Nyako anafahamika na wengi kwa juhudi zake kusaidia wasanii ambao hujipata taabani.

Nyako huwasaidia kuchangisha pesa kuanza maisha upya au kujinyanyua maishani.

Kupitia video yake aliyochapisha kwenye mtandao wa Tiktok mnamo Oktoba 31, 2023, mtengenezaji huyo wa maudhui aliwahimiza mashabiki wake kuwathamini wazazi wao kila wakati wakiwa wangali hai.

“Sijawahi kuzungumza kumhusu mama mzazi. Yeye ndiye amefanya ninaweza kuketi hapa. Utotoni mwangu niliishi sana katika shule ya bweni. Wakati nilimaliza shule, mama alikuwa ameaga dunia. Kwa hivyo, sina kumbukumbu bora kumhusu. Hivyo ndivyo hali ilivyokuwa,” akaeleza Nyako.

Nyako aliendelea kufichua kumpoteza baba na dadake aliyekuwa na umri wa miezi 12. Wawili hao waliaga kutokana na makali ya ugonjwa uo huo uliosababisha kifo cha mamake.

“Wakati huo, hakukuwa na dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo, na niliwapoteza wote,” aliendelea kusema.

Dadake aliyekuwa akimfuata mwenye umri wa miaka 12, pia alifuata mkondo huo, licha ya kutumia dawa za kupunguza makali ambazo anasema zilidhoofisha figo.

Wema wake wa kusaidia Brian Chira na mwanahabari Kimani Mbugua kwa kuwatafutia pesa walipolemewa na maisha umesifiwa sana.

Brian Chira alitumia pesa hizo kugharimia kulipa nyumba naye mwanahabari Kimani, akipokea pesa hizo alinuia kuazisha maisha upya pamoja na kazi.

  • Tags

You can share this post!

Wakenya sasa wageukia unga wa ‘kisiagi’ kupunguza...

Serikali kutuma polisi wa Coast Guards Ziwa Victoria

T L