• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 10:55 AM
Zari amtia wivu Diamond kwa kuolewa na ‘kibenten’

Zari amtia wivu Diamond kwa kuolewa na ‘kibenten’

NA MWANDISHI WETU

ZARI Hassan almaarufu The Bosslady, aliyekuwa mpenziwe mwanamuziki tajika wa Bongo Diamond Platnumz, alifunga ndoa na Shakib Cham.

Video zilizoenea mitandaoni zilionyesha wawili hao wakisherehekea uhusiano wao kwa ndoa. Harusi hii ya kisasa ni ya mara ya kwanza kwa soshiolaiti huyo.

Licha ya wawili hao kutofautiana kiumri kwa angalau miaka 10, Zari hapo awali ameonekana kutotishiwa na utofauti huo.

Amewakejeli na kuwasuta wanaompiga vijembe kwa kuwa katika uhusiano na mwanamume aliye mdogo kuliko yeye.

Zari aliyevalia rinda jeupe, alionekana mwenye furaha nyingi akivishwa pete na mpenziwe.

Kabla ya uhusiano huu na Shakib, Zari alikuwa amevishwa pete na marehemu Ivan Sswemwanga na Diamond lakini hawakufanya harusi.

Msanii Diamond Platnumz. PICHA | MAKTABA

Zari ambaye pia ni mfanyabiashara, ana watoto watano – wawili na Diamond na watatu na Sswemwanga – ambao walikuwepo kwenye harusi.

Uhusiano wa Zari na Shakib ulianzia wakiwa Afrika Kusini miaka michache iliyopita huku wakifanya harusi ya Kiislamu (Nikah) Aprili 16, 2023.

  • Tags

You can share this post!

Kinaya Nairobi ikipanga kununua maboti kudhibiti athari za...

Adhabu kali kwa wanaoficha dola za Amerika na kusababisha...

T L