• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 7:50 PM
Zari ashobokea shabiki aliyetapeliwa Sh24,000

Zari ashobokea shabiki aliyetapeliwa Sh24,000

NA FRIDAH OKACHI

MFANYABIASHARA mashuhuri wa Uganda, anayeishi Afrika Kusini, Zari Hassan amefichua mazungumzo yake na shabiki mmoja ambaye alitapeliwa pesa na mtu aliyetumia jina la soshiolaiti huyo.

Screenshot iliyochapishwa na soshiolaiti huyo, inaonyesha ujumbe kutoka kwa shabiki anayedai kulaghaiwa kwa ahadi angerudishiwa pesa hizo maara tano. Shabiki huyo alituma R3000 hii ikiwa ni sawa na Sh23,978 pesa za Kenya.

Shabiki huyo alikuwa amemtumia Zari ujumbe kwenye mtandao wa WhatsApp akitaka amrudishie R15,000 sawa na  Sh119,895 za Kenya.

Kulingana na chapisho la soshioliti huyo, alibainisha hafahamu kabisa alichokuwa akizungumzia.

“Hujambo, pesa zangu ziko wapi? Nahitaji pesa hizo tena ulisema nikilipa R3000 nitapokea R15,000 baada ya siku tatu. Nikiangalia kwenye akaunti yangu sioni chochote,” alisema shabiki.

Tafadhali nitumie pesa zangu, nimemaliza kufanya hivyo. Nitumie tu R3k zangu. Nilikuambia hizo pesa niliomba za uwekezaji na wewe unaomba pesa zingine. Tafadhali nirudishie pesa zangu,” aliongeza shabiki.

Zari alimshauri shabiki huyo kurudi alipoanzia mazungumzo ya kufanya dili ya kupata pesa mara tano baada ya ‘kuwekeza’. Alibainisha katika siku za nyuma aliwahi kuwaonya watu kuwa waangalifu na matapeli wanaofanya biashara mtandaoni kwa kutumia jina lake.

“Mbona wapumbavu wote mnapoibiwa ndio mnapata namba au barua pepe yangu?” Alimjibu Zari kwenye ujumbe.

“Kila siku nawaonya kuhusu walaghai kwenye mtandao lakini nyote hamsikii. Sina biashara na wewe hata kidogo. Nitatumia ujumbe huu kuwaonya wengine,”alikamilisha chapisho lake kwenye ukurasa wa WhatsApp.

Soshiolaiti huyo ambaye alikuwa mpenziwe mwanamuziki Diamond Plantnumz alishangaza mashabiki wake, kutokana na juhudi zake kuhakikisha mumewe Shakib na Diamond kukutana ana kwa ana. Hii ni baada ya Diamond kuzuru Afrika Mashariki kukutana na wanawe.

Zari aliendelea kuchapisha picha za wanawe wawili aliopata akiwa na Diamond pamoja na mtoto wake Tanasha Donna na kuwaita wanawe.

“Hao ni familia yangu. Ni watoto wangu,” alichapisha.

  • Tags

You can share this post!

Ziara ya Mfalme kuibua hekaheka wanaharakati wakimtaka...

Rais Ruto azindua simu ya mwananchi iliyotengenezwa nchini

T L