• Nairobi
  • Last Updated May 17th, 2024 8:50 AM
Zuchu adai Diamond ndiye mwanamume wa kwanza kumpa burudani chumbani

Zuchu adai Diamond ndiye mwanamume wa kwanza kumpa burudani chumbani

NA WINNIE ONYANDO

MWANAMUZIKI kutoka nchini Tanzania Zuhura Othman Soud almaarufu Zuchu, amefichua kuwa Naseeb Abdul almaarufu Diamond Platnumz ndiye mwanamume wa kwanza kumpa burudani chumbani.

Katika video iliyosambaa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, mwanamuziki huyo alidai kuwa Diamond ndiye mwanamume wa pekee ambaye amewahi kushiriki naye mapenzi.

Hii ni baada ya Zuchu kuulizwa idadi ya wanaume alioshiriki nao uroda akiwa na Diamond.

“Mpaka sasa ni wanaume wangapi umeshawahi kujienjoi kimapenzi? Zuchu alisoma swali aliloandikiwa kwenye karatasi.

“Mmoja tu,” Zuchu alijibu huku akimkumbatia Diamond na kuanza kumbusu.

“Pekee yake, pekee yake,” Zuchu alisisitiza.

“Hakuna mwingine. Wewe unamjua mpenzi wangu mgani? (Hakuna mtu. Unamfahamu mpenzi mwingine yeyote niliyewahi kuwa naye?” Zuchu aliuliza.

Hata hivyo, alisema kwamba Diamond naye ameshiriki mchezo wa huba na wengi.

“Hilo swali ni bora ukimuuliza yeye (Diamond),” Zuchu alisema.

Naye Diamond alipoulizwa swali hilo, alidai kwamba hajawahi kushiriki ngono na mwanamke yeyote isipokuwa Zuchu.

“Zuchu ndiye wa kwanza,” Diamond alisema na kumfuata Zuchu kwenye chumba.

Lakini ikumbukwe kwamba Diamond amewahi kuzaa na Zari Hassan, Hamisa Mobetto na Tanasha Donna.

Wawili hao awali walikuwa wakisema hawako kwenye uhusiano wa kimapenzi jambo ambalo wengi hawakuliamini.

Lakini kadri siku zinavyosonga ndivyo inaonekana penzi likipamba moto.

  • Tags

You can share this post!

Mzae bila wasiwasi tupate watu wa kutupigia kura –...

Fountain Gates ya TZ yamsajili mshambulizi Topister Situma...

T L