• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Mzae bila wasiwasi tupate watu wa kutupigia kura – Gachagua

Mzae bila wasiwasi tupate watu wa kutupigia kura – Gachagua

NA WINNIE ONYANDO

NAIBU Rais Rigathi Gachagua amewashauri wakazi wa Kericho kuendelea kuzaana.

Akizungumza Ijumaa kwenye hafla ya mazishi ya wakili Vincent Kipkoech Mutai, mwanawe mbunge wa Kipkelion Mashariki Mhe. Joseph Cherorot Kimutai, Bw Gachagua alisema kuwa wakazi wa eneo hilo wasiingilie kasumba ya kuzaa watoto wawili na kukomea hapo.

“Sisi tulipotoshwa na Wazungu,” akasema Bw Gachagua.

Aidha, alisema wakati wake umekwisha lakini wale ambao bado hawajapata watoto wanapaswa kukusudia kuwa na watoto zaidi.

“Wacha tujaze hii dunia, si Mungu ataangalia hawa watoto? Watoto ni baraka… sita, saba, nane tisa hapo… Mkikosa hawa watoto rais na mimi tutapigiwa kura na nani? Acha tujaze hii dunia kwa sababu hata Biblia inasema tujaze. Watoto watapata chakula, watasoma na mambo yatakuwa sawasawa,” Gachagua akasema huku umati ukiangua kicheko.

Hii si mara ya kwanza Bw Gachagua kuwataka Wakenya kuzaa watoto wengi.

Mnamo 2022, wakati wa mazishi ya kakake, John Reriani, Gachagua alisema Wazungu waliwahadaa Waafrika kwa kuwashauri dhidi ya kupata watoto wengi.

“Nadhani baadhi yetu hatukuwa na busara sana… Wazungu walipokuja walituambia tuzae watoto wawili tukakubali,” alisema.

  • Tags

You can share this post!

Gachagua asema kazi yake kubwa ni kuzuia watu fulani...

Zuchu adai Diamond ndiye mwanamume wa kwanza kumpa burudani...

T L