• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
DKT FLO: Nakerwa na hali ya mchumba wangu kukoroma anapolala

DKT FLO: Nakerwa na hali ya mchumba wangu kukoroma anapolala

Mpendwa Daktari,

Mchumba wangu hukoroma sana anapolala, jambo ambalo hunikera sana. Suluhu ya kudumu kwa tatizo hili ni ipi?

Ezrah, Nairobi

 

Mpendwa Ezrah,

Kukoroma husababishwa na sauti inayotokana na mtikiso wa tishu za njia ya juu ya kupitisha hewa shughuli hii inapoendelea, hasa ikiwa njia hii ikiwa nyembamba.

Wembamba wa njia hii waweza tokana na kuziba kwa pua, uzani mzito, kuvimba kwa findo, kuvimba kwa kikoromeo au matatizo mengine, majeraha au maradhi yanayoathiri umbo la uso au shingo.

Aidha, hali hii yaweza tokea ikiwa haujalala vizuri.

Mbali na hayo, una uwezekano mkubwa wa kukoroma ikiwa wewe ni mwanamume, ukiwa mjamzito, au ukiwa mchovu.

Ili kudhibiti hali hii, usinywe pombe inapokaribia wakati wa kulala, jiepushe na matumizi ya dawa za kuchochea usingizi, dumisha uzani unaofaa, usiwe na mazoea ya kulala chali-lala kwa upande, tibiwa ikiwa una tatizo la pua kuziba, unapolala hakikisha kwamba kichwa chako kimeinuliwa.

Pia, usivute sigara, pata usingizi wa kutosha, badilisha mito yako mara kwa mara na unaweza tumia vifaa vya kuhakikisha kwamba njia ya kupitisha hewa inasalia wazi.

Mbali na hayo, unashauriwa kufanyiwa uchunguzi na mtaalamu wa masikio, pua na koo (ENT)na pia upigwe picha za eksirei ili kutambua nini hasa kibaya na upate matibabu.

  • Tags

You can share this post!

KWPL: Ni mbio za farasi wawili, Gaspo Women na Vihiga Queens

Bewa la MKU Rwanda sasa ni Mount Kigali University

T L