• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 12:18 PM
DOMO: Sanaa ya injili ya Kenya hakika imejaa vibonzo

DOMO: Sanaa ya injili ya Kenya hakika imejaa vibonzo

NA MWANAMIPASHO

NISHASEMA hapa mara nyingi tu kwamba ingawaje wakati mwingine huwa nakubaliana na wengi wenu kuwa Eric Omondi ni mwehu, kuna nyakati huwa napenda mashobo yake.

Toka juzi msela katrendi kinoma baada ya kichaa chake kumtuma kuwatoa rangi wanamuziki wa injili.

Alidai kuwa Willy Pozze aka Bwana Mkunaji kazi yake kubwa siku hizi ni kuzurura maeneo ya vyuo vikuu akiendesha Mercedes Benz huku akivizia vibinti vya chuoni.

Akamshukia Ringtone Apoko aliyedai kuwa msela kazi yake ni kuwabadilisha mademu kama nepi ya mtoto wa miezi mitatu.

Hakumwacha DK Kwenye Beat ambaye kama mnakumbuka miaka michache, alitrendi kwa madai kuwa alihadaa demu fulani na kuishia kumwambukiza kisonono.

Basi nilikuwa najua watu waliojazajaza kama DK ndio hawawezi kazi, khuh kumbe wanaweza mpaka kupitiliza. Madai haya yalizama ila kwa namna kesi ilivyofuatiliwa kulikuwa na ukweli kwa asilimia fulani.

Ila kama ilivyo ada mshikwa na ngozi ndio mwizi na hakuna mwizi aliyewahi kukiri kuwa mwizi. Lakini nakumbuka msela akiomba msamaha.

Waliomsapoti kipindi anaomba msamaha ni DJ Mo na mke wake, msela mwingine wa injili ambaye skendo zake za michepuko akiwa kwenye ndoa, zinatosha kuunda Reality Show ya kipekee. Kwa bahati nzuri yeye hakutajwa.

Na mwingine wa injili aliyekwepa shobo la Eric ni Mr Seed. Huyu ni mwingine. Juzi tena kaamsha mapepo ya baby mama wake Liz Sonia.

Miaka kadhaa iliyopita alimkagua mtoto wa uswahilini, akammiminia masharubati yake na kitanda hakikuzaa haramu. Bwana mdogo sasa ana miaka saba na kulingana na mamake Sonia, Mr Seed, mpandaji mbegu hajawahi kumshughulikia hataa.

Nilitia kicheko juzi Liz alipoposti meseji zao za WhatsApp. Sikuamini msela anayejigamba kuwa anajenga jumba la vyumba vinane, alimtumia Sonia Sh5,000 kama fedha za matunzo halafu kesho yake akaamka kumwomba Sonia amkopeshe Sh2,000 eti nyumbani hakuna unga.

Liz alipomwanika miezi miwili iliyopita na jamaa akaulizwa kunaendaje, msela alidai eti baby mama alikuwa akisaka kiki. Kiki ya nini sasa wakati Sonia sio msanii?

Mwanaume wa aina gani huyu tena anayejifanya kuwa mwinjilisti kazi kuzalisha na kusepa. Kumbuka Liz sio wa kwanza, 2021 yupo binti Msomali aliyemwanika kuwa msela alimzengua vile vile akamwahidi kumpa vyote vilivyopo chini ya jua, na kama jina lake akampanda mbegu.

Kawaida msela aliruka ila binti alitoa uthibitisho wa meseji msela akiwa amemtumia Sh4,000 huku akimshinikiza atoe ujauzito ule. Stori taratibu ikazama. Kama kuna dume lenye roho tisa kama za paka kwenye kustahimili skendo za michepuko basi atakuwa huyu.

Ila pia nyie mademu huwa mnaniangusha sana, dogo ana nini kinachowafanya kutokwa uchizi kiasi cha kumwachia awapande mbegu, au kwa sababu staa? Mmh! Haya bwana.

Yote hayo tisa, kumi, Eric kwenye hili, kagonga ndipo, tasnia ya injili Kenya imejaa vibonzo, bora kabisa waache kujiita wasanii wa injili. Sio kwa kero zao. Tena wengine wana ujasiri wa kujiita vioo vya jamii wakati unakutana nao wamepiga mtepesho, suruali yataka kudondoka sababu makalio ya hata kushikilia uzi wa suruali hawana.

Wangwana mnihukumu mtakavyo ila tujifunze kuambiana ukweli. Kama ukiumwa, nenda ukasikie vibaya na kule.

  • Tags

You can share this post!

KASHESHE: Rapa Wakazi amtoa rangi Babu Tale

AFC yaibebesha Talanta mabao, Posta Rangers na Wazito...

T L