• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 5:59 PM
DOMO: Vera, makalio si kitu kipya!

DOMO: Vera, makalio si kitu kipya!

NA MWANAMIPASHO

KWA kweli mambo ni mengi masaa ndio machache.

Kuna msela mmoja pale Twitter anajiita Billy The Goat. Ana ufuasi mkubwa sana kule. Kijiji kizima kwa kweli. Watu zaidi ya 250,000 wanamfuata kutokana na kupendezwa na mambo yake.

Jumatano aliandika ujumbe mzito akikusanya matukio yote yaliyotrendi Twitter. Alizungumzia ishu ya Wakili Nkatha aliyetrendi kwa kumkejeli mkufunzi wa kampuni yao ya uwakili. Walimtuma kupeleka stakabadhi fulani kwa wateja wao, huyo mwanafunzi akaamua kutumia Uber.

Nkatha akaona hilo ni bonge la ishu akaja kulalamika Twitter. Wadau wakabaki kumpasha. Mwenyewe nashindwa alitaka huyo mwanafunzi atumie chopa au?

Kisha kulikuwa na stori ya yule mwanahabari Kimani Mbugua kuachwa na mamake kwenye hospitali ya Mathare inayoaminika kuwa ndio nyumbani kwa watu wenye akili taahira. KOT wakakesha nayo. Halafu kuna ile stori ya cool kid Emma Too anayeishi ndani ya klabu. Jamani mambo mengine sielewi. Halafu sasa kuna ishu ya huyo Ruger kulipwa Sh3.6 milioni kwa shoo ya ovyo kule Meru.

Kwa kweli mambo ni mengi. Ila naomba tumzungumzie shangazi yenu Vera Sidika. Aisee mimi bwana Shikwekwe alishanichosha zamani. Nimeziona kiki kibao ila kiki ya kungo’a makalio eti ndio usukume ngoma, hiyo nayo mpya.

Jamani nipo hapa najiuliza kama ngoma ile imefanikiwa. Subiri nikacheki ina views ngapi mwanzo…. Aah! Nyimbo imejitahidi sana ina views 421,000+ ndani ya hizi siku sita toka imeachiwa… Mmh!

Wimbo wenyewe kusema kweli ni utumbo tu. Wala hamna kitu pale. Yeyote atakuwa mpumbavu kumwalika Vera shoo akatumbuize wimbo huo maana watu watasinzia.

Ila kwa nini aende umbali kama huo. Huyu binti anasema yeye hufanikiwa kutokana na chuki za watu. Sasa hapa kuna kufanikiwa kweli maana ninakuhakikisha hii ngoma haitafikisha views hata milioni. Pengine tuipe miaka 10 kutoka leo.

Bado sielewi ni kwa nini aliamua kiki ya makalio. Atakuwa anamisi kuzungumziwa kama ilivyokuwa zamani alipofanya mazoea ya kujaza kurasa za magazeti na blogu. Sasa hivi kaisha utamu, hana ladha tena na makeke yake.

Kama ni makalio wametokea masoshiolaiti wengi na ma Instagram Babez wenye vibuyu vya uhakika waliofanya wadau kumsahau. Sasa basi siku nyingine atang’oa nini ili kusukuma wimbo wake ujao. Katumia silaha ya kipekee aliyokuwa nayo kuchoma tena kwa wimbo wa ovyo. Toka ametokea hadi leo hii, Shikwekwe ameishi kutegemea kibuyu chake kutrendi.

Nakumbuka kuna kipindi aliposti nusu uchi ilimuradi azungumziwe. Leo kawa mama anajitahidi kuwa na heshima kidogo kwa binti yake mchanga. Hivi nikuulize Princess Asia atakapotimu umri, kisha akutane na uwongo wa mamake, Vera atamwambia alifanya hivyo kusukuma muziki?

Shikwekwe anahitaji kuanza kuwaza mambo mengine au kiki za kiutuuzima zaidi. Hata Kim Kardashian kwa sasa kachoka. Nina uhakika hawezi kuposti tena uchi eti ndio alipwe.

Kwa miaka 40 na, anaelewa kabisa alishapita uzuzu wa miaka ya nyuma. Tatizo kamwacha nyuma dada yetu huyu. Kweli murife kaamua hatakimbia…

  • Tags

You can share this post!

KASHESHE: Vannyboy arusha jiwe

KNUT yataka serikali iajiri walimu 58,000

T L