NA SINDA MATIKO
MWANAMUZIKI Rayvanny karusha jiwe gizani kwa kudai kwamba toka ameondoka WCB Wasafi, sanaa yake imekua hata zaidi.
Vannyboy anasema toka amchoree giza Diamond Platnumz mumiliki wa WCB, anahisi amekua kimuziki sana kiasi cha akili zake kufunguka pakubwa.
“Ukweli sijutii kuondoka, sijutii maamuzi yangu. Kwenye lebo yangu kila kitu wa kuulizwa ni mimi sababu mimi ndiye bosi mkubwa ninayehusika na mambo yote ikiwemo kuwalipa wasanii. Hii imenisaidia kupevuka zaidi.”