• Nairobi
  • Last Updated May 3rd, 2024 11:33 PM
Faida za mbegu za maboga

Faida za mbegu za maboga

Na MARGARET MAINA

[email protected]

MBEGU za maboga zina protini ya kutosha na ya muhimu zaidi mwilini. Pia zina madini ya zinki, copper, magnesium na chuma.

Mbegu hizi unaweza kuzitafuna zikiwa zimekaushwa kwenye jua, ama kuzikanga kwa mafuta lakini pia mbegu hizi unaweza kuzisaga kupata unga ambao utakuwa unachanganya kwenye juisi yako ya matunda au uji angalu vijiko viwili kwa siku .

Kinga ya kisukari

Mbegu za maboga zina Nicotinic Acid, Trigonelline, na D-Chilo-Inositol ambayo husaidia kushusha kiwango cha sukari kwenye mwili na kuthibiti kazi za Insulini hivyo kuwa kinga na kuwapa nafuu watu wenye kisukari ambapo mbegu hizi husaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza kiasi cha sukari kwa wagonjwa.

Ulaji wa mbegu za maboga hushusha kiwango cha sukari mwilini, hupunguza kiasi cha mafuta yasiyofaa mwilini mbegu hizi pia hulinda viungo vya mwili dhidi ya athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na uwepo wa sukari nyingi pamoja na kuharibu mafuta yanayoleta athari mbalimbali hasa kwenye mishipa ya moyo kutokana na uwepo wa wingi wa kemikali za flovonoids , tannins, phenols pamoja na saponins ambazo husisimua ngongosho liweze kuzalisha homoni nyingi za insulini ambazo ndizo hutumika katika kulinda kiasi cha sukari.

Huongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha

Mbegu za maboga huongeza maziwa kwa mama anayenyonyesha.

Mbegu hizi zina protini nyingi bora itokanayo na mimea isiyo na madhara pia zina Omega 3 mama mjamzito anaweza kutumia mbegu za maboga na kuwa na uhakika wa kutoa maziwa ya kutosha kwaajili ya mtoto.

Tatizo la upungufu wa damu

Mbegu za maboga ni chanzo kizuri cha madini ya chuma hivyo kuwa msaada kwa watu wanaosumbuliwa na upungufu wa damu unaosababishwa na kupungua kwa madini ya chuma, tafiti zinasema kua kula vyakula vyenye madini ya chuma kila mara kunasaidia kuongeza madini ya chuma kwa watoto, vijana wanawake wanaonyonyesha na kwa akina mama wajawazito.

Zinaondoa msongo wa mawazo

Unashauriwa kutafuna mbegu za maboga kwa kua zina kimeng’enya muhimu sana kwa kutuliza mawazo kiitwacho tryptophan na Amino asidi nyingine muhimu zinazohusika katika utengenezaji wa homoni ya serotonin ambayo ni katika kuratibu matendo kadhaa katika ubongo.

You can share this post!

Vyakula hivi si vya kuliwa kila mara

Faida ya korosho kwa mwili wa binadamu