• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 10:50 AM
Hii imeenda! Samidoh atambulisha mpango wake wa kando, Karen Nyamu, kuwa mkewe

Hii imeenda! Samidoh atambulisha mpango wake wa kando, Karen Nyamu, kuwa mkewe

NA SAMMY WAWERU  

EDDAY Nderitu, ambaye ni mke wa kwanza wa mwimbaji wa nyimbo za Mugithi, Samuel Muchoki maarufu kama Samidoh huenda akaangukiwa na ‘pigo’ jingine la moyo. 

Hii ni baada ya Samidoh kukiri kutambua mpango wake wa kando, seneta Karen Nyamu kuwa mke wake wa pili.

Wawili hao wamekuwa kwenye uhusiano haramu, licha ya Samidoh kuwa mume wa Edday.

Mahusiano hayo aidha yamepelekea kupata watoto wawili.

Edday na Samidoh wamejaaliwa watoto watatu, ikizingatiwa kuwa Edday ndiye mke halali anayetambulika – Yaani mke aliyetolewa mbuzi (mahari).

Kupitia video, mwanamuziki huyo anaskika akimuita Karen kwa majina ya mama wa mwanawe kuhutubia watu, hali ambayo inatafsiriwa kama kumtambua rasmi kuwa mkewe.

Alikuwa ameandamana naye katika hafla ya mazishi Nyandarua. Muimbaji huyo ambaye pia ni askari, alikuwa anazungumza kwa lugha ya Kikuyu.

“Uka nyima wa Wairimu ugeithanie…Oka ugeithie adu, tucoke tucokerie MC, (Njoo Mama Wairimu usalimiane…Usalimie watu kisha turudishie mfawidhi maikrofoni,” Samidoh anasikika akisema kwenye video hiyo.

Naye Karen anaonekana kuwa mwepesi wa kuamka, na kusalimu waombolezaji.

“Bwana asifiwe, Bwana asifiwe tena, tusalimiane kwa salamu za hewani (ishara ya mkono), mimi naitwa Karen Njeri, kama mlivyosikia mimi ni seneta nchini humu.”

Utambuzi wa Karen kama mama Wairimu (jina la mama Samidoh alilopewa mtoto waliopata pamoja, kwa mujibu wa mila, itikadi na tamaduni za jamii ya Agikuyu) ni ishara mwanamuziki huyo anamtambua mpango wake wa kando kama mke rasmi.

Mwezi uliopita, Edday aliandika kupitia akaunti yake ya Facebook ujumbe ulioashiria kuchoshwa na uhusiano haramu kati ya Samidoh na Karen.

Mama huyo aidha alilalamikia kukosewa heshima na mume wake, ikikumbukwa kuwa Samidoh na Karen wameweka paruwanja mitandaoni kuhusu uhusiano wao.

Isitoshe, wawili hao wamekuwa wakipapurana mitandaoni wanapotofautiana.

Desemba 2022 katika kilabu Dubai, Karen alizua drama wakati Samidoh akitumbuiza mashabiki wake.

  • Tags

You can share this post!

Yesu wa Tongaren adai huiona mbingu kila siku asubuhi

Makala ya kwanza ya michezo ya ufukweni Kenya ni Machi...

T L