• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 12:18 PM
Kajala akiri kuchumbia mwanasiasa

Kajala akiri kuchumbia mwanasiasa

Na JOHN KIMWERE

HATIMAYE mwigizaji wa Bongo Movie, Frida Masanja Kajala amefunguka sababu iliyopelekea kutengana na aliyekuwa mchumba wake msanii Rajab Abdul Kahali maarufu Harmonize.

Akizungumza na wanahabari siku chache zilizopita baada ya kutua hapa nchini, Kajala alisema lengo lake kuu kufika Kenya lilikuwa kujumuika na mashabiki wake kwa ajili ya hafla ya kuwasaidia wasiojiweza (charity event).

Baadaye akizungumza kwenye kipindi cha Mambo Mseto, mwigizaji huyo aliweka wazi kuwa aliyekuwa mchumba wake alionekana alimchukulia poa tu na kudai ndio sababu iliyochangia kuachana naye.

Alidokeza kuwa mwenzake alianza kuonyesha dalili hizo licha ya kwamba mwanzoni walionyeshana kuwa katika mahusiano ya kweli.

“Binafsi nilikuwa napendelea nyakati zote kuwa wote (pamoja) lakini ilifikia kipindi fulani ambapo niligundua kuwa ni kama Harmonize alinizoea sana na ndiyo sababu ya kanichukulia poa,” Kajala alisema.

Aliongeza kuwa kamwe hawezi kumlaumu maana yeye ni kijana mdogo na pengine alihitaji nafasi ya kufanya mambo yake ya pembeni.

Kuhusu kama alimpata amechepuka alisema “hilo siwezi kulizungumzia.”

Mahusiano na mwanasiasa Kenya

Aidha akijibu swali la endapo ana mchumba mwingine huku akichangia kicheko ila hakufunguka kabisa alisema kuwa yupo kwenye mahusiano mengine na mwanasiasa mmoja hapa Kenya.

“Kwa sasa nina mchumba mpya kwa kipindi cha miezi miwili, ni mwanasiasa hapa Kenya ila kamwe siwezi kumtaja,” Kajala akasema.

Aidha alidokeza kuwa amepania kumzalia mdogo wake binti yake, Paula muda tu wakati atakapompata mwanaume anayefaa.

Kajala akizungumzia hatua ya kuachana na Harmonize wakati wa kipindi cha kwanza kabla hawajarudia alisema alirudi baada ya kuombwa msamaha na pia alikuwa anapenda Harmonize sana.

Mapema Aprili, Harmonize alikiri kuachana kwake na Kajala kulimpelekea kutunga kibao ‘Single Again’ ambacho imeibuka kuwa moto.

Bosi huyo wa lebo ya Konde alifunguka kuwa alighani kibao hicho kama njia ya kujifariji baada ya kutemana na mchumba wake huyo.

”Tulikuwa tunapendana sana na Kajala ambapo baada ya kunitema ilibidi nitunge fataki hiyo ili kujituliza kutokana na majeraha ya kuachwa,” Harmonize akasema.

 

  • Tags

You can share this post!

Marion Mwende Muema: Nalenga kuwa nyota gwiji katika...

Kinaya gavana kuteua waziri kuvalia kiatu cha ugavana...

T L