• Nairobi
  • Last Updated May 2nd, 2024 4:42 PM
Mapenzi yanoga, Madam Boss, Akothee afichua humpigia simu mpenziwe mzungu saa tisa alfajiri

Mapenzi yanoga, Madam Boss, Akothee afichua humpigia simu mpenziwe mzungu saa tisa alfajiri

NA SAMMY WAWERU

MWANAMUZIKI Esther Akoth maarufu kama Akothee amefichua kwamba humpigia simu mchumba wake mzungu alfajiri na mapema kila siku kumjulia hali alivyolala usiku kucha.

Muimbaji huyo wa kibao maarufu Give it To Me, alifichua Jumanne kwamba kuzungumza na mpenzi wake mzungu saa tisa alfajiri ni ratiba yake.

Mchumba wake anayemtambua kama Omosh anaishi ng’ambo, na humtembelea, na Akothee tayari amemtambulisha kwa familia yake.

Mapema mwaka huu, pamoja na jamaa za mpenziwe walitembelea wazazi wake katika Kaunti ya Migori, hatua iliyofasiriwa kama kuhalalisha uhusiano wao.

“Mtu wa kwanza ninayezungumza naye ninapoamka ni mume wangu, saa kumi na moja asubuhi saa za Kenya sawa na saa tisa alfajiri nchi anayotoka,” Madam Boss akaandika kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook.

Mwanamuziki Akothee akiwa shambani mwake. PICHA / HISANI

Kwa mujibu wa chapisho hilo, Akothee yuko eneo la mashambani ambako huendeleza kilimo.

Mama huyo wa watoto watano ni mfugaji hodari wa nguruwe, na ufichuzi wake kuhusu saa anazozungumza na mchumba wake unaashiria alikuwa kwenye shamba lake la mboga.

Akothee anaonekana akihamisha na kupanda miche ya mboga, huku akikagua kabichi na pia kuvuna sukuma wiki, akidokeza kwamba mazao hayo ni ya nguruwe.

Alielezea jinsi alivyo na bahati kama mtende kuwa mpenzi wa mchumba wake mzungu.

Muimbaji Akothee akipanda mboga shambani mwake. PICHA / HISANI

“Nina bahati kuwa na Bw Omosh. Ninamkumbusha jinsi alivyo wa maana, ninaenzi kuwepo kwake katika maisha yetu,” akajivunia muimbaji huyo wa kibao tajika cha Kula Ngoma.

Akimmiminia sifa chungu nzima, alifichua baadhi ya mambo aliyomfanyia ikiwemo kununulia familia yake jenereta akidokeza kwamba kijiji anakotoka cha Rakwaro hakijakuwa na stima siku tatu, akalijaza mafuta pamoja na gari lake hadi pomoni kabla kurejea ng’ambo.

“Kwa nini nising’ae?” akauliza mashabiki wake.

Kupitia chapisho hilo, Akothee alisema mwanamke anajivunia mwanamume anayetunza urembo wake, kumpa motisha na kumsaidia anapohitaji.

Esther Akoth maarufu kama Akothee akikagua kabichi. PICHA / HISANI
  • Tags

You can share this post!

Wito kwa wanahabari waangazie maswala muhimu kuhusu afya,...

KNCHR yaanza uchunguzi kuhusu uvunjaji wa haki za binadamu...

T L