Na MARGARET MAINA
TAMBI ni chakula ambacho kwa kawaida humchukua mpishi muda mfupi sana kukipika.
Muda wa matayarisho: Dakika 5
Muda wa mapishi: Dakika 15
Walaji : 2
Vinavyohitajika
Tambi pakiti 2
Tui nusu kikombe
Hiliki punje 4
Zabibu kikombe ¼
Maji lita 1
Arki ya vanilla kifuniko 1
Maelekezo
Vunja vunja tambi zako weka kwenye sahani.
Twanga hiliki zako.
Weka maji kwenye sufuria.
Teleka sufuria kwenye meko maji yapate moto vizuri.
Mimina tambi kwenye maji ya moto halafu uache yachemke kwa dakika nne hadi zilainike kisha mimina kwenye chujio zikauke maji.
Mimina tui kwenye sufuria. Weka hiliki na acha tui lichemke.
Kisha weka arki, zabibu na mimina tambi zako.
Changanya tambi zako kwa kutumia mwiko kugeuzia tambi zenyewe. Geuza tambi zako mpaka zikaribie kukauka kisha funika na uache zikauke.
Zikikauka, pakua tayari kula kwa choche unachopenda.
Muhimu
Usichemshe tambi sana mpaka zikavurugika.
Usiweke tambi haraka kabla tui halijachemka.
Hakikisha tambi zinakauka vizuri kabla ya kuzipakua.