• Nairobi
  • Last Updated May 14th, 2024 10:01 PM
MAPISHI KIKWETU: Jinsi ya kuandaa tambi (noodles)

MAPISHI KIKWETU: Jinsi ya kuandaa tambi (noodles)

Na MARGARET MAINA

[email protected]

TAMBI ni chakula ambacho kwa kawaida humchukua mpishi muda mfupi sana kukipika.

Muda wa matayarisho: Dakika 5

Muda wa mapishi: Dakika 15

Walaji : 2

Vinavyohitajika

Tambi pakiti 2

Tui nusu kikombe

Hiliki punje 4

Zabibu kikombe ¼

Maji lita 1

Arki ya vanilla kifuniko 1

Maelekezo

Vunja vunja tambi zako weka kwenye sahani.

Twanga hiliki zako.

Weka maji kwenye sufuria.

Teleka sufuria kwenye meko maji yapate moto vizuri.

Mimina tambi kwenye maji ya moto halafu uache yachemke kwa dakika nne hadi zilainike kisha mimina kwenye chujio zikauke maji.

Mimina tui kwenye sufuria. Weka hiliki na acha tui lichemke.

Kisha weka arki, zabibu na mimina tambi zako.

Changanya tambi zako kwa kutumia mwiko kugeuzia tambi zenyewe. Geuza tambi zako mpaka zikaribie kukauka kisha funika na uache zikauke.

Zikikauka, pakua tayari kula kwa choche unachopenda.

Muhimu

Usichemshe tambi sana mpaka zikavurugika.

Usiweke tambi haraka kabla tui halijachemka.

Hakikisha tambi zinakauka vizuri kabla ya kuzipakua.

You can share this post!

NLC yazuiwa kununua ardhi hewa ya Sh668m

KCB, Posta Rangers zatafuta huduma za winga wa Mathare John...

T L