• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 9:55 AM
KCB, Posta Rangers zatafuta huduma za winga wa Mathare John Mwangi

KCB, Posta Rangers zatafuta huduma za winga wa Mathare John Mwangi

Na JOHN KIMWERE

KLABU ya Mathare United huenda itakosa huduma za winga wake John Mwangi anayeripotiwa kuwindwa na timu mbili, KCB na Posta Rangers ambazo hushiriki Ligi Kuu ya Shirikisho la Soka la Kenya (FKF-PL).

Mkataba wake Mwangi maarufu Mavado na klabu hiyo iliyotwaa taji la Ligi Kuu mwaka 2008 unaelekea kumalizika.

Itakumbukwa mwaka 2021 klabu tatu KCB, Wazito FC na Bandari zilijaribu kuwinda saini ya mchezaji huyo lakini alikaa ngumu kinyume na mara hii ambapo inadokezwa kuwa amepania kusaka makao mapya.

Duru zinaeleza kuwa kocha mkuu wa KCB, Zedekiah ‘Zico’ Otieno ameelezea kuwa analenga kutwaa huduma za mchana nyavu huyo.

Kwa upande mwingine inaelezwa kuwa uongozi wa Posta Rangers pia umepania kukutana na mchezaji huyo kabla ya wiki hii kukatika.

Posta Rangers tayari imenasa huduma za wachana nyavu wawili Patrick Otieno na Geoffrey Shiveka.

Pia imeachilia Dennis Oalo na Josphat Lopanga. Endapo mchezaji huyo atahama, itakuwa pigo kubwa kwa Mathare United ambayo inaendelea vibaya kwenye kampeni za Ligi Kuu msimu huu.

Mathare United ipo katika mduara wa kushushwa ngazi nafasi ya 17 kwa kuzoa alama saba sawa na Vihiga Bullets baada ya kushiriki mechi 16.

Aliyekuwa naibu kocha wa Wazito FC, John Kamau anatazamiwa kujiunga na Mathare United kujaza pengo la kocha Ezekiel Akwana aliyejiuzulu wiki iliyopita.

  • Tags

You can share this post!

MAPISHI KIKWETU: Jinsi ya kuandaa tambi (noodles)

Wauzaji pombe Kiambu wapunguziwa ada ya leseni kwa asilimia...

T L