NA MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 20
Muda wa mapishi: Dakika 40
Walaji: 3
Vinavyohitajika
kilo 1 nyama ya mbuzi
punje 4 kitunguu saumu; sagasaga
kijjiko ½ cha thyme
juisi ya limau
mtindi
kijiko 1 cha sosi ya soya
ndizi 15 za kijani kibichi (zimechujwa na kukatwa vipande vipande)
nyanya 3
maji
vitunguu maji 2, katakata vipande vipande
majani ya giligilani
pilipili mboga
chumvi
mafuta ya kupikia
Maelekezo
Changanya mtindi wako wa kawaida, sosi ya soya au uyoga, thyme na maji ya limau.
Baada ya yote kuchanganywa, ongeza kitunguu saumu chako kilichosagwa na uchanganye. Mara baada ya kusambazwa sawasawa, mimina yaliyomo kwenye nyama yako ya mbuzi iliyokatwa na uiruhusu ikae kwa si chini ya muda wa saa tatu.
Weka nyama pamoja na mchanganyiko wako kwa sufuria mekoni ili vichemke kwa pamoja. Usiioshe nyama maana kwa kuacha hivyo itageuka kuwa nzuri na yenye ladha zaidi. Ongeza kikombe 1 cha mchuzi wa nyama ya nyama ya ng’ombe/ mboga au maji kidogo ili kuhakikisha nyama inakuwa laini.
Baada ya nyama kuchemka, weka kando. Katika kikaango tofauti, ongeza vitunguu, tangawizi na pilipili na kaanga. Vitunguu vyako vikishakuwa laini, weka nyanya yako kisha vikaange kwa takribani dakika tano au hadi vilainike.
Ongeze nyama, changanya, kisha, ongezea viungo upendavyo. Funika na baada ya dakika tano, epua.
Chemsha ndizi kwa dakika 15, kisha zikaange kwa mafuta na kitunguu na nyanya.
Ongezea mtindi na ufunike kisha uache chakula kiive kwa dakika tano hivi.
Ongezea majani ya giligilani kwa juu, epua na upakue. Furahia chakula chako.