• Nairobi
  • Last Updated May 14th, 2024 10:01 PM
MAPISHI KIKWETU: Pancakes za ndizi

MAPISHI KIKWETU: Pancakes za ndizi

NA MARGARET MAINA

[email protected]

PANCAKES za ngano na ndizi hutengeneza kiamsha kinywa chenye afya na muhimu kwa familia nzima. 

Muda wa kuandaa: Dakika 10

Muda wa mapishi: Dakika 15

Walaji: 3

Vinavyohitajika

  • Kikombe 1 cha unga wa ngano
  • Kijiko 1 cha poda ya kuoka
  • Kijiko ½ unga wa mdalasini
  • Chumvi kijiko ¼
  • Yai 2
  • Ndizi 3 zilizoiva kabisa
  • Vijiko 3 vya asali
  • Vijiko 2 vya siagi iliyoyeyuka
  • Kijiko ½ cha vanilla
  • Mafuta ya kupikia
Madonge ya kutengeneza pancakes za ndizi. PICHA | MARGARET MAINA

Maelekezo

Changanya viungo vyote kavu; yaani unga, poda ya kuoka, mdalasini na chumvi kwenye bakuli.

Katika bakuli lingine, ongeza sukari au asali au chochote kitamu unachotumia, mayai, maziwa, ndizi zilizopondwa kwa uma na siagi iliyoyeyuka. Koroga vizuri kwa pamoja.

Ongeza mchanganyiko wa viungo majimaji kwenye mchanganyiko wa viungo kavu.

Kwa kutumia kijiko cha mbao au mkono wako, changanya vizuri michanganyiko yako.

Weka kikaangio kwenye chanzo cha moto na usubiri hadi kiwe moto.

Ongeza mafuta kidogo ya kupikia, na ukitumia kijiko, ongeza mchanganyiko wako kwenye kikaangio.

Pika kwa dakika mbili au hadi pancake iwe na rangi ya hudhurungi kisha ipindue. Ongeza mafuta kidogo na acha pancake yako iive.

Rudia kwa mchanganyiko wote uliobakia upata pancakes za kutosha. Epua moja baada ya nyingine epua na upakue. Hakikisha unanyunyuzia kwa juu chokoleti, matunda au karanga.

You can share this post!

BORESHA AFYA: Baadhi ya faida za mwarubaini

Kalonzo alaumu Ruto kuhusu bei za juu za bidhaa

T L