• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 6:50 AM
MwanaTikTok Kevin Kinuthia ajivunia gari jipya akiliita ‘Mtoto mwenye Baraka’

MwanaTikTok Kevin Kinuthia ajivunia gari jipya akiliita ‘Mtoto mwenye Baraka’

NA MERCY KOSKEI

MWANAMITANDAO maarufu wa TikTok Kevin Kinuthia amewaacha mashabiki wake vinywa wazi baada ya kusambaza video ya gari lake jipya – akilipa jina ‘mtoto mwenye baraka’.

Gari hilo la aina ya Nissan Note nyekundu alilipa jina Baby Blessing.

Katika video hiyo, iliyochapishwa Julai 14, 2023 kwenye mitandao yake ya kijamii, Kinuthia alionekana akitembea mbele ya gari huku akiwa amepambwa na kuvalia wigi na suti nyeupe.

Katika video hiyo, aliandika maneno haya: “Kwa sasa ni wakati wa mama na mtoto, karibu nyumbani Baby Blessing.”

Kinuthia pia alionekana akiwa ameketi kwenye kiti cha dereva, huku akijipiga picha – selfie.

Mashabiki na wafuasi wake walivamia chapisho hilo, wengi wakimpongeza kwa kununua gari.

Mwanamitandao huyo huiga maisha ya kike, ambapo hujipodoa na kuvalia mavazi ya wanawake.

  • Tags

You can share this post!

Julai 16: Waziri Kindiki aadhimisha siku maalum ya kuzaliwa

Mbunge amsihi Prof Kindiki ajibwage kortini kutetea Mswada...

T L