• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 6:50 AM
Julai 16: Waziri Kindiki aadhimisha siku maalum ya kuzaliwa

Julai 16: Waziri Kindiki aadhimisha siku maalum ya kuzaliwa

NA SAMMY WAWERU

WAZIRI wa Usalama wa Ndani Prof Kithure Kindiki Jumapili, Julai 16 aliadhimisha siku maalum ya kuzaliwa.

Akifahamika kwa majina kamili kama Abraham Kithure Kindiki, Waziri huyu mkakamavu alizaliwa Julai 16, 1972 katika Kaunti ya Tharaka Nithi.

Prof Kindiki aliungana na waumini wa Kanisa la Katoliki la Kaanwa, Igambang’ombe, Chuka, Kaunti ya Tharaka Nithi ambapo keki kuadhimisha miaka 51 ilikatwa.

Kabla kuteuliwa Waziri wa Usalama wa Ndani, Prof Kindiki alikuwa amehudumu kama Seneta wa Tharaka Nithi kati ya 2013 hadi 2022.

Ni mmoja wa mawaziri wa serikali ya Rais William Ruto wanaosifiwa kutokana na utendakazi wake wa kipekee hasa kukabiliana na uhalifu nchini. s

  • Tags

You can share this post!

Ashangaza kuambia korti bangi humpa motisha kulima shambani...

MwanaTikTok Kevin Kinuthia ajivunia gari jipya akiliita...

T L