NA MWORIA MUCHINA
KAKAKUONA (Pangolin) ndiye mnyama wa pekee duniani ambaye ngozi yake ina magamba kama ngozi ya nyoka.
Hula mchwa na wadudu wengine na hawana meno.
Humeza mawe ili kusaidia kusaga chakula tumboni.
Anaweza kula zaidi ya mchwa 20,000 kwa siku.
Hujipinda kama mpira wanapovamiwa na adui na ndio wanyama wanaouzwa kwa zaidi kwenye soko la magendo. Hii ni kwa sababu raia wa mojawapo ya mataifa ya Bara Asia huamini ngozi na nyama yao huponya magonjwa kadhaa.