• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 3:31 PM
AMINI USIAMINI: Samaki anayewinda kwa kutema maji kama risasi

AMINI USIAMINI: Samaki anayewinda kwa kutema maji kama risasi

NA MWORIA MUCHINA

SAMAKI kwa jina archer, huwinda wadudu na viumbe wengine wadogo kwa kutema maji kutoka kwa midomo yao kama risasi.

Samaki hao, huvizia wadudu wanapokuwa wametulia kwenye mashina ya miti na majani ya miti karibu na maji.

Hulenga mdudu huyu kwa kuchiririza maji hayo bila kukosea shabaha. Wadudu wanapoanguka juu ya maji kutokana na shambulio hilo, samaki huwanasa na kuwala.

  • Tags

You can share this post!

Wanafunzi wa vyuo vikuu kushiriki katika mashindano...

Mung’aro azindua miradi iliyoanzishwa na Kingi

T L