• Nairobi
  • Last Updated April 28th, 2024 3:31 PM
PAUKWA: Bahili akausha boda na kuipapia probox

PAUKWA: Bahili akausha boda na kuipapia probox

NA ENOCK NYARIKI

MATATU aliyoabiri Bwana Bahili ilitoka kwenye stani ya Kanyumba ikateleza kwenye barabara ya kuelekea Birika.

Kufumba na kufumbua jicho, ilikuwa imewasili kwenye klabu cha Burudani. Kondakta aligotagota kioo kwa sarafu na gari likatia nanga ili baadhi ya abiria washuke.

“Aisee pilot, shusha Kambimoto,’’ Bahili alimwambia dereva wa matatu.

Dereva alishika breki na kulielekeza gari kandokando ya barabara. Bwana Bahili alichukua kifurushi chake alichokiweka chini ya miguu na mkoba wake ambao ulipumzika kwenye mapaja yake akashuka. Punde tu alipovuka barabara, vijana wawili, wafanyabiashara wa bodaboda, waliwasha pikipiki na kuziendesha kuelekea alikokuwa Bahili huku wakishindana kumbeba.

“Wanangu, si leo. Leo, nitatembea!’’ Bahili aliwakatisha tamaa.

Kutoka kwenye kituo cha Kambimoto, kuna kichochoro chembamba ambacho kinapita kwenye joho la miti kabla ya kuungana tena na barabara ya moramu ya Oloilie ambayo imepinda mfano wa nyoka.

Bahili aliamua kufuata kichochoro hicho ili kuhepa biwi la mavumbi la magari ya kubeba mawe.

Muda si muda, aliungana tena na barabara ya moramu. Gari geni la probox lilitia nanga mbele yake na kupiga honi. Bahili aliwapungia mkono; ishara kwamba hakutaka kubebwa maadamu alikuwa anakaribia mwisho wa safari. Dereva wa Probox alishuka na kumwambia Bahili:

“Mzee, tunajua umekaribia unakokwenda lakini tunataka kukupa lifti na kukuuliza jambo.’’

Bahili aliambua nyayo na kuikaribia probox.

You can share this post!

Uhuru asema hatageuza msimamo kuhusu Raila

Kidero aahidi kuonyesha ODM kivumbi akisaka ugavana Homa Bay

T L