• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 12:44 PM
Riggy G kuongoza hafla ya utoaji mahari ya mbunge Murang’a

Riggy G kuongoza hafla ya utoaji mahari ya mbunge Murang’a

MWANGI MUIRURI Na WANGU KANURI  

NAIBU wa rais Rigathi Gachagua ataongoza katika mazungumzo ya ulipaji mahari kati ya mbunge wa Mathira Eric wa Mumbi na Betty Maina, mwakilishi wa wanawake katika Kaunti ya Murang’a.

Habari hii ilidhibitishwa na Wa Mumbi mnamo Jumatatu, akizungumza kupitia runinga ya Inooro.

Akimsifia atakayekuwa bibi yake, Bw Wa Mumbi alisema kuwa yupo tayari kuishi kama mke na mume na mpenziwe.

“Wiki hii nitakuwepo Murang’a kwa matayarisho kabla ya siku hiyo kubwa ambayo itawafanya wengi kuhisi wivu kwa jinsi nitamuendea mpenzi wangu,” akasema.

Mbunge wa Mathira Eric wa Mumbi na mchumba wake Betty Maina, ambaye ni mbunge mwakilishi wa wanawake Kaunti ya Murang’a. PICHA / HISANI

Vile vile, Wa Mumbi aliongeza kuwa ibada hiyo ya utoaji mahari utakuwa mchanganyiko wa itakadi anazofuata kama Mkristu na kama mzee wa baraza.

Hata hivyo, mbunge huyo alisema kuwa hatishwi na pesa atakazoitishwa kwenye mazungumzo hayo kwani hakuna thamani inayoweza kumtosheleza Bi Betty.

Huku akiwamiminia sifa wazee wa Mathira kwa kuwa matajiri na wasiohofu chochote, Bw Wa Mumbi alisema, “Tumefuga mbuzi na wema wetu hautoshelezwi na chochote.”

“Hivi sasa hakuna siri ya kuwa ni mimi ninaishi na mtoto wenu na jioni ifikapo, tunarudi nyumba moja ambayo tunaita yetu,” akasema.

Aliongezea, “Jua linapochomoza sote wawili huenda njia tofauti ili tutoe huduma kwa wakazi wa Murang’a na Mathira lakini tunapatana jioni kwa nyumba yetu.”

Huku urafiki wao na uhusiano wao ukisheheni wakati wa kampeni ambapo Bw Wa Mumbi alikuwa akieleza wakazi kuwa Bi Betty anatosha, ‘Betty E Sawa,’ mbunge huyo aliapa kuwalea watoto wao kwa upendo.

 

  • Tags

You can share this post!

CAS Kimani Ngunjiri taabani kwa kumpiga mtu risasi

Wakazi Kisumu watakiwa kuwa macho kuhusu Kipindupindu

T L