• Nairobi
  • Last Updated May 20th, 2024 6:55 PM
Tanzia, Shatta Bwoy akimuaga mkewe kwa kuwekelea nywele kwenye jeneza

Tanzia, Shatta Bwoy akimuaga mkewe kwa kuwekelea nywele kwenye jeneza

NA MERCY KOSKEI

MTANGAZAJI wa runinga ya Citizen Shatta Bwoy alimheshimu mkewe kwa njia maalum wakati alipokuwa akizikwa siku ya Jumamosi July1, 2023 katika Kaunti ya Makueni.

Hafla ya mazishi ilihudhuriwa na wafanyakazi wenzake kutoka shirika Royal Media Services, familia na marafiki.

Huku akimmiminia sifa za mwisho, Shatta alisema kuwa aliahidi mkewe kwamba siku moja atakata nywele kwa ajili ya kozi ya maana.

Alieleza waombolezaji kuwa mkewe amekuwa mtu mwenye upendo na ulinzi sana na kuwa alipoanza kufuga ‘dreadlocks’ alimtaka ziwe na maana.

“Nilimwambia (Mke Becky) siku moja nikipata jambo la maana, nitakuwa nakata nywele moja baada ya nyingine kuhakikisha kuwa sitasahau siku hiyo na kwa bahati mbaya siku niliyoahidi inaanza na wewe,” Shatta Boy alieleza.

Baada ya kukata nywele zake 31, Shatta aliwekelea juu ya jeneza la mkewe.

“Mama Yaeli ukiondoka unaenda na sehemu ya taji hilo nakupenda. Nitawapenda watoto wetu kama ulivyonitaka, nitawalinda na kuhakikisha kuwa mimi ni baba bora milele ulivyotaka,” alisema.

Mtangazaji huyo wa redio pia alikumbuka maneno ya mwisho ya mkewe kabla ya kuaga dunia, akisema kuwa alimwambia: “Baba Jael nenda nyumbani uchunge watoto, mimi napumzika.”

Katika hafla ya kumuaga mkewe, alifichua alimwambia: “Nitafanya hivyo, nitawalinda. Nakupenda Sana, lala salama.”

 

  • Tags

You can share this post!

Wachuuzi Londiani warejea barabarani licha ya ajali...

Mbunge Gachagua: Walioandamana kwa kuvalia sufuria kichwani...

T L