• Nairobi
  • Last Updated May 11th, 2024 11:02 AM
UDAKU: Harmonize adai amekosa kolabo na Davido kwa sababu ya Diamond

UDAKU: Harmonize adai amekosa kolabo na Davido kwa sababu ya Diamond

NA RAJAB ZAWADI

NI kawaida sana kwa wasanii kunyimana kolabo kwa sababu mbalimbali.

Wapo wasanii ambao hutoza hela kufanya kolabo na wenzao na wapo wale watakukatalia tu kwa sababu pengine vaibu lako haliwabambi.

Miongoni mwa wasanii ambao ni wepesi kusaka kolabo na wasanii aina aina ni Harmonize Rais wa KondeGang Music Label.

Sasa juzi akitia stori kwenye podcast moja hivi, mzee baba alifunguka na kudai kwamba amekuwa akiifukuzia kolabo na mkali wa Afrobeat Davido kwa muda sasa sema bado hajafanikiwa.

Harmonize anadai sababu yake kufeli kuipata kolabo na Davido imechangiwa pakubwa na bosi wake wa zamani Diamond Platnumz.

“Wakati nilipokuwa USA Davido alinitafuta na kuniomba tufanye remix ya ‘Single Again’. Ilibidi nimtumie kipande changu ili naye aingie kipande chake, lakini cha kushangaza mpaka leo hii Davido amenikaushia na hata hakunijibu,” anadai Harmonize.

Kulingana naye, ukakasi uliopo kati yake na Simba aka Chibu Dangote, ndio sababu maalum iliyomfanya Davido kumchunia.

“Hivyo sababu ya yote ni nifu letu kwa sababu alihisi (Davido) kama akifanya kolabo na mimi huenda itakuwa chuki kwa wengine,”

Ifahamike kuwa ushikaji wa Diamond na Davido ulianza zaidi ya miaka saba imepita, sasa nyota huyo wa Bongo akiwa bado sio staa mkubwa kama alivyo.

Kipindi akiwa anapambana kujulikana nje ya mipaka ya Tanzania, Diamond aliamua kufanya kolabo na Davido ambaye kwa wakati huo ndiye alikuwa msanii aliyekuwa akitrendi sana Nigeria na Afrika kwa ujumla.

Diamond alikiri nusura afilisike baada ya kulazimika kukopa benki mamilioni ya pesa ili kufanikisha kolabo yake na Davido kwenye remix yake ya Number One, 2014.

Bosi huyo alifichua kutumia zaidi ya Sh3.3 milioni kipindi hicho kufanikisha kolabo hiyo ikiwa ni gharama tu ya utengenezaji wa ngoma hiyo pasi na kuongeza gharama zingine za kando, kama vile za hotelini, mavazi na usafiri – kusafirisha timu yake nzima kwenda kushuti na kuandaa ngoma Nigeria na Afrika Kusini vile vile.

Diamond alisema alilazimika kusafiri zaidi ya mara kumi kwenda Nigeria kufanikisha mradi huo.

Toka kipindi hicho mpaka sasa, anakuwa staa wa haiba yake, ushikaji wake na Davido umedumu.

Kwa maana hiyo, ili kolabo itoke basi huenda Harmonize akahitaji baraka kutoka kwa Diamond kumruhusu Davido.

Na hilo kutokea ni sawa na kuupaka upepo rangi maana chuki kati ya Diamond na Harmonize kwa sasa ipo kwenye levo nyingine.

  • Tags

You can share this post!

Waititu: Nilipotoshwa na uongozi wa UDA

Waziri Owalo amfuta kazi meneja wa KBC Samuel Maina

T L