• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 7:50 AM
Waziri Kindiki – Sikuwa nakumbuka nilizaliwa Julai 16 

Waziri Kindiki – Sikuwa nakumbuka nilizaliwa Julai 16 

NA SAMMY WAWERU

WAZIRI wa Usalama wa Ndani Kithure Kindiki alizua ucheshi katika Kanisa la Katoliki la Kaanwa, Igambang’ombe/Chuka, Tharaka Nithi mnamo Jumapili, Julai 16, 2023 alipohoji hakuwa anakumbuka siku yake ya kuzaliwa. 

Prof Kindiki alizaliwa Julai 16, 1972 katika Kaunti ya Tharaka Nithi.

Akizungumza baada ya kushiriki ibada ya misa Kanisa la Katoliki la Kaanwa, Waziri Kindiki alisema majukumu aliyopewa na Rais William Ruto hayampi muda kukumbuka baadhi ya mambo.

“Hii wizara ina majukumu kibao hata sikuwa nakumbuka leo (Jumapili, Julai 16 ni siku maalum ya ukumbusho wa kuzaliwa kwangu…Nimejulia hapa wakati nimeona keki,” Prof Kindiki aliambia waumini, matamshi yaliyofuatwa na kicheko.

Cha kuvunja mbavu zaidi, Waziri alisema alisaidiwa na viongozi walioandamana naye kutoka Kaunti ya Tharaka Nithi kufanya hesabu ya idadi ya miaka yake.

“Hata hesabu ya miaka tumefanyia hapa, nikaona kumbe nimefikisha miaka 51,” Prof Kindiki alielezea.

Kabla kuteuliwa kujiunga na Baraza la Mawaziri la Rais William Ruto, Bw Kindiki alihudumu kama Seneta wa Tharaka Nithi kati ya 2013 hadi 2022.

Waziri pia ni wakili mwenye tajiriba ya muda mrefu.

 

  • Tags

You can share this post!

Mbunge amsihi Prof Kindiki ajibwage kortini kutetea Mswada...

Wanafunzi 8 Bungoma wanyakwa kufuatia njama kuteketeza bweni

T L