• Nairobi
  • Last Updated May 5th, 2024 5:50 AM
TUSIJE TUKASAHAU: Chokoraa wangali tishio la usalama

TUSIJE TUKASAHAU: Chokoraa wangali tishio la usalama

VIJANA wanaorandaranda mitaa, maarufu kama chokoraa, wangali tishio la usalama katika barabara kadha katikati mwa jiji la Nairobi, ishara ya kufeli kwa juhudi za kuwaondoa.

Visa vya watu, haswa wanawake, kuhangaishwa na hata kupokonywa mikoba na vijana hawa hutokea katika barabara zenye shughuli nyingi kama zile za Tom Mboya Road, Kirinyaga Road na River Road.

Lakini safu hii inamkumbusha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Huduma za Jiji (NMS) Luteni Jenerali Mohamed Badi kwamba mnamo Februari 25, 2019 aliahidi kuondoa kero ya chokoraa katikati mwa jiji Nairobi na mitaani.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Huduma za Jiji (NMS) Luteni Jenerali Mohamed Badi. PICHA | MAKTABA

Aliahidi kuanzisha mpango wa kuwaondoa vijana hao barabarani na kuwapeleka katika vituo vya kurekebisha tabia ili wapewe mafunzo mbalimbali ya yenye manifaa kwao maishani.

Vituo hivyo ni kama vile Bahati Reception Centre, Pumwani Reception Centre, Joseph Kangethe Reception Centre na hata Shirika la Vijana kwa Huduma za Taifa (NYS).

Muda wa kuhudumu kwa NMS ukitarajiwa kukamilika Machi mwaka huu, Jenerali Badi asije akasahau kutimiza ahadi yake ya kuondoa chokoraa, na familia za barabarani, jijini Nairobi.

  • Tags

You can share this post!

DCI yatahadharisha al-Shabaab imetuma magaidi kushambulia

Migawanyiko Ukambani siasa zikinoga

T L