• Nairobi
  • Last Updated May 19th, 2024 9:01 PM
TUSIJE TUKASAHAU: Dkt Ruto akifanikiwa ajenge mabwawa ya Arror na Kimwarer lakini pia awape wakazi fidia

TUSIJE TUKASAHAU: Dkt Ruto akifanikiwa ajenge mabwawa ya Arror na Kimwarer lakini pia awape wakazi fidia

MNAMO Jumatatu, Naibu Rais William Ruto aliahidi kufufua mradi wa ujenzi wa mabwawa ya Arror na Kimwarer akishinda urais na kuunda serikali Agosti.

“Kwa mapenzi ya Mungu baada ya kushinda uchaguzi Agosti 9, tutaendelea na ujenzi wa mabwawa haya mawili. Miradi hii itawasaidia wakazi kupata maji kwa mifugo, kilimo na uzalishaji wa kawi ili kuchochea maendeleo katika eneo hili,” Dkt Ruto akasema alipokuwa akiendesha kampeni katika Kaunti ya Elgeyo Marakwet.

Lakini Naibu Rais alisahau kuangazia suala la fidia ya zaidi ya wakazi 50,000 ambao waliahidiwa kulipwa fidia ya Sh6 bilioni kwa kutoa ardhi zao kwa serikali kwa ajili ya ujenzi wa mabwawa hayo.

Juzi, wakazi hao walifanya maandamano mjini Iten wakishinikiza walipwe fidia hiyo waliyoahidiwa mnamo 2019.

Watu hao walihamia maeneo mengine licha ya kukwama kwa miradi hiyo, iliyofaa kugharimu Sh63 bilioni, kutokana na sakata ambapo Sh21 bilioni ziliporwa kabla ya kazi kuanza.

  • Tags

You can share this post!

Viongozi wa Kiislamu wataka Magoha afutwe kazi kwa matamshi...

Tusker yatoa masharti kuachilia kipa Matasi

T L