• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 11:39 AM
TUSIJE TUKASAHAU: Rais afahamu IDPs wangali wanahangaika

TUSIJE TUKASAHAU: Rais afahamu IDPs wangali wanahangaika

MNAMO Agosti 5, 2019 wakati wa mazishi ya aliyekuwa Gavana wa Bomet Joyce Laboso, Rais Uhuru Kenyatta aliahidi kuwa serikali yake itakamilisha mpango wa kufidia wakimbizi wa ndani kwa ndani (IDPs) walioachwa nje ya mpango uliopita.

“Tunaelewa kuna IDPs ambao hawakuwa wamelipwa fidia. Ningependa kuwahakikishia kuwa tutalipa kila mmoja wao; wawe Nakuru, Laikipia, Bomet, Nyandarua au Kericho. Wale waliopewa ardhi ya serikali pia watasaidiwa kujenga makazi mapya,” akasema mjini Bomet wakati wa ibada ya wafu.

Lakini inaonekana serikali ya Rais Kenyatta haijatimiza ahadi hiyo huku muhula wake wa pili na wa mwisho uongozini ukielekea kukamilika.

Kwa mfano, wakati huu zaidi ya familia 1,500 za IDPs hao, ambao ni waathiriwa wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu wa 2007, bado wanaishi kwenye mazingira duni katika wadi ya Salama eneobunge la Laikipia Magharibi, Kaunti ya Laikipia.

Wengi wa watoto wao hawaendi shuleni kutokana na ukosefu wa nafasi na walimu wa kutosha katika shule ya msingi ya Kianjogu, iliyoko karibu na eneo ambako wanaishi katika nyumba za mabanda.

  • Tags

You can share this post!

WANDERI KAMAU: Tunatumia vibaya uhuru wa kidemokrasia...

TAHARIRI: Mashindano ya Kip Keino ni faida kuu kwa taifa...

T L