MNAMO Juni, 2021 Waziri wa Elimu George Magoha alipunguza karo katika shule za upili za mabweni baada ya wizara yake kufupisha mwaka huu wa masomo kwa wiki tisa; kutoka wiki 39 hadi 30.
Kwenye taarifa iliyotumwa kwa walimu wakuu na Katibu katika Wizara hiyo Julius Jwan, karo katika shule za kitaifa ilipunguzwa kutoka Sh55,000 hadi Sh45,000. Shule za ngazi ya wilaya zilitakiwa kupunguza karo kutoka Sh45,000 hadi 35,000.
Lakini, Profesa Magoha ajue kwamba walimu wamekiuka mwongozo huu na wanaendelea kuwatoza wazazi karo ya juu.