• Nairobi
  • Last Updated May 8th, 2024 8:55 PM
Antonio Rudiger aagana rasmi na Chelsea na kuyoyomea Uhispania kuchezea Real Madrid

Antonio Rudiger aagana rasmi na Chelsea na kuyoyomea Uhispania kuchezea Real Madrid

Na MASHIRIKA

BEKI mzoefu wa Ujerumani, Antonio Rudiger, 29, amejiunga rasmi na Real Madrid kwa mkataba wa miaka minne baada ya kuagana na Chelsea bila ada yoyote.

Atatambulishwa rasmi kwa wasimamizi, wachezaji na mashabiki wa Real mnamo Juni 2022 ugani Santiago Bernabeu.

Nyota huyo ameyoyomea jijini Madrid kuvalia jezi za mabingwa wa Ligi Kuu ya Uhispania (La Liga) na wafalme wa Klabu Bingwa Ulaya (UEFA) baada ya kukataa kurefusha muda wa kuhudumu kwake ugani Stamford Bridge.

Rudiger alijiunga na Chelsea mnamo 2017 baada ya kubanduka kambini mwa AS Roma nchini Italia kwa Sh4.3 bilioni. Anaondoka Stamford Bridge baada ya kuchezea Chelsea mara 203 huku akipachika wavuni mabao 12 na kushindia kikosi hicho Kombe la FA, taji la Champions League, Europa League, Uefa Super Cup na Kombe la Dunia.

Kwa mujibu wa Chelsea, Rudiger ni miongoni mwa “wachezaji wazalendo zaidi kuwahi kuvalia jezi zao katika miaka ya hivi karibuni.”

Rudiger aliyekuwa pia akiwaniwa na Bayern Munich ya Ujerumani, alikataa ofa ya mshahara wa zaidi ya Sh30 milioni kwa wiki ili kusalia Chelsea.

Mbali na Rudiger, Chelsea wanatazamiwa pia kukatiza uhusiano na beki matata raia wa Denmark, Andreas Christensen anayehusishwa pakubwa na Barcelona. Beki na nahodha Cesar Azpilicueta amerefusha muda wa kuhudumu kwake kambini mwa Chelsea kwa mwaka mmoja zaidi.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Italia na Ujerumani watoshana nguvu katika pambano la...

11 wafa ajalini Kitui wakitoka hafla ya kulipa mahari

T L