• Nairobi
  • Last Updated May 4th, 2024 10:15 PM
Arteta anataka mzee Wenger arudi Arsenal

Arteta anataka mzee Wenger arudi Arsenal

Na MASHIRIKA

MKUFUNZI wa Arsenal Mikel Arteta amefichua kuwa analenga kuhakikisha kuwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo Arsene Wenger, 72, anarejea klabuni kwa majukumu au wadhifa tofauti.

Mhispania Arteta alisema kuwa ameshajadiliana na Wenger kuhusu hilo. Kocha huyo aliongoza Arsenal kushinda mataji matatu ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) pamoja na saba ya FA kwa kipindi cha miaka 22 aliyodumu ugani Emirates.

Aidha, Arteta mwenyewe alicheza miaka mitano chini ya Wenger kikosini Arsenal.Mhispania huyo alirithi mikoba ya Unai Emery mnamo Desemba 2019, miezi 19 baada ya Wenger kuondoka katika klabu ya Arsenal msimu wa 2017-2018.

You can share this post!

Conte anamvizia difenda Bailly wa United

Tusker, Gor zalenga ushindi Caf kesho

T L