Na MASHIRIKA
MKUFUNZI wa Arsenal Mikel Arteta amefichua kuwa analenga kuhakikisha kuwa aliyekuwa kocha wa timu hiyo Arsene Wenger, 72, anarejea klabuni kwa majukumu au wadhifa tofauti.
Mhispania Arteta alisema kuwa ameshajadiliana na Wenger kuhusu hilo. Kocha huyo aliongoza Arsenal kushinda mataji matatu ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) pamoja na saba ya FA kwa kipindi cha miaka 22 aliyodumu ugani Emirates.
Aidha, Arteta mwenyewe alicheza miaka mitano chini ya Wenger kikosini Arsenal.Mhispania huyo alirithi mikoba ya Unai Emery mnamo Desemba 2019, miezi 19 baada ya Wenger kuondoka katika klabu ya Arsenal msimu wa 2017-2018.