• Nairobi
  • Last Updated May 18th, 2024 11:39 AM
Conte anamvizia difenda Bailly wa United

Conte anamvizia difenda Bailly wa United

Na MASHIRIKA

MKUFUNZI wa Tottenham Hot Spurs Antonio Conte ameandaa mazungumzo na mabosi wake, kuhusu uwezekano wa kumsajili beki wa Manchester United, Eric Bailly.

Mwanadimba huyo raia wa Ivory Coast amekuwa akilishwa benchi United, na amecheza kwa dakika 45 pekee ligini msimu huu. Inasemekana Conte ni shabiki mkubwa wa difenda huyo.wa mlinzi huyo na anapanga kumshawishi aigure United ili ajiunge na Spurs.

Nahodha wa United Harry Maguire, na Raphael Varane pamoja na Victor Lindelof ambao walisajiliwa mnamo Agosti wamekuwa wakipendelewa kuliko Bailly.Mwanasoka huyo mwenye umri wa miaka 27 mara nyingi amekuwa akisumbuliwa na jeraha tangu atue ugani Old Trafford miaka mitano iliyopita.

Amecheza mara 17 pekee katika misimu mitatu iliyopita.Hata hivyo, majarida kadhaa nchini Uingereza yamedai kuwa Conte ni shabiki wa mlinzi huyo na anapanga kumshawishi aigure United ili ajiunge na Spurs.

You can share this post!

Kisasi kilimchochea akanyuka Mcuba na kushinda dhahabu

Arteta anataka mzee Wenger arudi Arsenal

T L